Oooh ni kweli Mungu ambariki sana. Namfahamu sana na hata baada yz Upadrisho wake alitutembelea nyumbani. Mimi naamini Mungu snapoamua kukuita kuwa mtumishi wake hata ukimbie lazima utaitika tu. Ni kama Yona alivyokuwa anakataa maagizo ya Bwana hadi kumezwa na samaki akajikuta Ninawi. Pd Richard Mungu aendelee kukutumia sawasawa na wito wake aliokuitia. ( Mimi ni Rose Vitalis Swai) Historia yako inatia moyo,na kutokukata tamaa.
Hongera sana pd Laswai, mimi nimepata bahati ya kukufahamu ukiwa Karatu. Nafahamu ulivyo kuwa mchapakazi, mnyenyekevu na mcha Mungu sana. Mungu azidi kukulinda kukutunza na kukubariki.
Mzuri sana ndungu, Baba Mungu apewe sifa kwa uwito wako wa upekee yenyi kuonyesha ukubwa na uwezo wake Baba Mungu. Kitume njema ndungu. D.alphonse Marie.
Hongera Sana Baba padre kwa wito, ningeshauri hii historia ya Baba ingewekwa kwenye kumbukumbu za kanisa ili iweze kuwahamasisha vijana kuitikia miito mbalimbali
Hongera sana baba kwa kusikia wito bora na hakika historia yako ni mafunzo tosha kwa vijana wetu.itapendeza waandishi wakakufuata huko uliko ili kumbukumbu hizi zikae vizuri
Namkumbuka sana Laswai wakati sisi tunaanza Form one Sanu Seminari yeye alikuwa kiranja wa Chakula.Kiukweli huyu mtu ni mvumilivu na mstaarabu sana.Ni mwenye hekima na busara sana wakati wote.Ni mtu wa kushauri pale mambo yanapokuwa hayaendi sawa.Natamani ningepata no zake nimsalimu
Hata huku kwetu sumbawanga Diocese kuna Padre aliacha kazi ya serikali na akaenda seminary akiwa na umri mkubwa... Alipewa jina la YOHANE MARIA VIANE.. MWENYEZI MUNGU KAMCHUKUA😭 katika Miaka5+ ya Utume wake... MUNGU amrehemu... 🙏🙌