"Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa. Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu. Mtu huyo akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka. Na Petro, akamkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, tutazame sisi. Akawaangalia, akitarajia kupata kitu kwao. Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende. Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vyake vikatiwa nguvu. Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka ruka na kumsifu Mungu" (Matendo 3:1-8)
"Maana umri wake yule mtu aliyefanyiwa ishara hii ya kuponya ulipita miaka arobaini."(Matendo 4:22)
11 окт 2024