CHAKULA BORA
1.Sasa ninahisi harufu ya chakula - harufu nzuri tena ya kipekee. Kweli ninahisi harufu ya kinywaji - kinywaji bora tena cha kipekee.
Amkeni wapenzi (twende) kule sebuleni, tuandamane sote (twende) tufike mezani. Tukamwone mpishi (huyo) aliye imara, tukamwone ni nani (huyo) anayesisimua Lo! (kumbe ni Yesu ametuandalia mazuri, tujitakase tushiriki chakula cha roho x2)
2.Kati ya wapishi wote ulimwenguni - sijawahiona mpishi kama Yesu. Anayeandaa chakula cha dhamani - kinachodumisha uhai siku zote x2
3.Kati ya wafalme wote ulimwenguni - sijawahiona aliyefanikiwa. Kuwaandalia watu wote karamu - akawashibisha pasipo ubaguzi x2
4 сен 2019