Juha Kalulu si jina geni, hasaa kama wewe ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili.Ni safu katika gazeti la Taifa Leo, inayoangazia, kibonzo mmoja machachari, na mkewe sara,na mbwa wao kwa jina tusker.wengi hasaa vijana wa jana walipenda sana katuni huyo, lakini mchoraji wake, wengi hawamfahamu. Mwanahabri wetu Joab Mwaura alimsaka mzee Edward Gitau mwenye umri wa miaka 82 ambaye kwa zaidi ya miaka sitini amekuwa akitayarisha safu ya Juha Kalulu bila kusita, na ndiye anayetupambia makala ya enzi zao.
14 окт 2024