Daah uyo tajiri mjinga sana kuliko ange tumia mawakili kupambana na uyo mwanamke angekaa nae amlipe angerizika ss akaona pesa zake zingeweza kupindisha sheria
Tajiri kakataaa kutoa rushwa wanamkomesha tu, miaka 20 mtu anaanza kujenga waziri wa aridhi alikuwa wapi adi mjengo umekwisha, ndio wanakuja kubomoa kwanini wasimkataze kujenga au huyo kashitaki huzi baada kuona mjengo tayari nn
Tatizo tunapata huruma baada ya kuon uvunjaji hatumfirii mwenye kiwanja amepitia mateso kiasi gani, huenda kashatukanwa sana na kudhihakiwa wakati akidai haki yake, miaka 20 angekuwa ameshafanya uwekezaji wake lakini ameishia kuhangaika, ukisema wapatane alipwe hapo wenye nguvu ya pesa watawahamisha wanyonge wote kwa kuvamia maeneo yao wakitegemea watawalipa fidia wakishtaki. Acha maamuzi magumu na machungu yafanyike
Ardhi mko hovyo sana, nyinyi ndo mlikuwa mkiwauzia watu wawili wawili viwanja Kwa nini msiwashauri waelewane? Kama ni haki hata aliyeuziwa mala ya pili nae ana haki. Watumishi wenu ndo wabovu, wabaneni waache hiyo michezo
Umeandika kwa akili na ufafanuzi mzuri sana... Hakuna kuhamisha mtu... Inatakiwa ivunjwe na amlipe hasara ya muda na faida alioipoteza kwa kunyimwa fursa ya kuwekeza
Hata huyo aliyejenga usikute alikuwa na hati. Ardhi kuna wakati walikuwa wanawapiga sana watu. Kiwanja kikikaa miaka 5 bila kujengwa wanamuuzia mtu mwingine. Ilitokea Sana Sinza
Jamani mingu yupo anayenda mambo kwa wakati sasa alitumia nguvu ya pesa kuchukuwa kiwanja kwa pesa kiko wapi, mungu analipa hapa hapa duniani, mungu azidi kukulinda waziri maana hapa duniani tunapita, tenda haki kabisa mungu atakurinda.
Mama kitomari hongera kw kumjua mmiliki,hii ni fundisho hapo mbez ,Afrikana wezi sana matajiri wanatumianpesa na kwenda Ardhi kuhonga hii iwe Fundi should
Mama kitomari nimemfahamu zaidi ya miaka 24 iliyopita na alikua mtumishi katika taasisi flani hivi mika ya 2001 hivyo A To z anamjua huyo dada naomi ndie mmiliki
Huyo anayebomoa na kijiko ukute anaishi kichochoroni ata bei ya msumari haijui, ila tafuteni suluhu za kibinadamu maana hapo itakua mmetengeneza uhasama mkubwa sana haswa familia yenye hiyo asset... Mtanguluzeni mungu
Wewe unajielewa kweli, au hata sheria unajua yaan mwizi akuibie halafu useme kwamba suluhisho itafutwe na vielelezo vimenyooka fikiri kabla y kuweka koment sheikh hii nchi ina sheria
Inauma sana kwann nyie kama viongoz bas msingeingilia kat hata huyo mwenye nyumba amlipe huyo mama au amtaftie eneo lingne amnunulie!! Kuliko kuvunja hyo nyumba Ina gharama sana jaman kuwen na huruma Bora huyo mama mngekubali amlipe!!
Miaka ishirini ni mingi sana msiwe na haraka majibu mtayapata tu ugali bado upo jikoni subirini wapakue ndio mtajua wa moto au wa baridii haki Ina maumivu😂
Shida sio kuelewana, wenye pesa ni mara chache kuwa wanyenyekevu, ebu umesmbiwa utamtambua yeye nani, umekosakoswa kufa. Sasa farao hasiyejua mema ya daudi kapatikana. Au godfather ardhi na serikalini kastaafu au kafa. Acha haki isimame. Utamtambua mimi ni nani hûwa ina mwisho. Tz tujifunza kutendeana haki.
ogopa sana neno linalo itwa haki, haki ni zaid ya sheria aise tujifunze ivyo hapo na bado, jerry fanya kazi yako bila kugeuka nyuma. watasema sana laikini usiku watalala. asante.
Sasa si mngempa hiyo nyumba naomi ailipie pole pole, hata mkiibomoa huyo noami si atakuja kujenga tena. Kama serikali imeshampa naomi umiliki basi wangekaa chini na kujadili kuhusu jengo na kukubaliana hata nusu hasara ilipwe kuliko kubomoa. Na unaweza kukuta mwenye nyumba na yeye hana kosa ni tamaa za madalali tu, ndiyo wamemungiza katika matatito.
Kweli kabisa uku kwetu Toangoma Mtaa wa Masaki katika viwanja vya serikali, maeneo mengi ya wazi yameuzwa na serikali ya mtaa na maafisa ardhi Temeke, na bado wanaendelea kuuza . Mbona serikali hipo kimya .
Hili zoezi ni zuri na lifanyike nchi nzima.Na kwa hiki kilichotokea hapo kwanza washikwe wote waliohusika kumuuzia kiwanja huyo mvamizi,na huu mfumo wa madalali uchwara inabidi upigwe marufuku kisheria.Kama mtu anataka kiwanja anunue direct kwa mmiliki halali au serikalini.Mambo ya udalali kwenye ardhi ni utapeli wa waziwazi.Mweshiwa Waziri Slaa hebu liangalie hili kwa kina.
Sijapenda kwa kweli. Ilitakiwa busara itumike kwa sababu huu uzembe hata serikali wamehusika. Kuliko kubomoa nyumba ni bora ingetumika busara ya kumlipa huyo naomi kiasi ambacho angekiridhia akanunue kiwanja kingine
Miaka 20..je ni mawazir wangapi wamepita?hata yule mama wamwanza alietumbuliwa alikuwa mwizi tuuu. Ona kazi inavyokwenda sasa...mungu akuweke waziri na moyo huo ulionao na akuripe kadir ya utendavyo haki❤
Uyo mwenye njumba angee Kaa nae uyo mama wayaongee amununulie sehemu amkabizi ampe na pesa kidogo kikubwa izidi samani ya kiwanja kuliko kuvunjiwa njumba kubwa ivyo duuuu
Hapa inaonyesha huyu tajiri alakataa kumlipa mwenye kiwanja akatumia nguvu ya fedha sasa amejua kwamba majonzi ya mtu si mazuri serikali simamieni haki za watu binadamu wote ni sawa
Ck zote mtenda akitendewa huhisi kaonewa na mkuki kwa ngurue kwa binadam mchungu miaka 20 we kuweza? Muda wote huo nani anafidia hasara hiyo? Lazima tukubali matokeo.
Jamani ninyi mbona mnaona hiyo nyumba? Hivi mnajua maumivu ya kuporwa mali yako? Yaani ardhi ya kwako alafu ichukuliwe na mtu mwingine. Kwa sababu ana fedha
Nyinyi viongozi hajielewi hata Kidogo kweli mnashindwa kuwaweka Sawa hawa watu wawili2 tu. Sio poa Tanzania inawana siasa wakongwe wengi tu Mngekwenda hata kwa Mizengwe pinda mkawakutanisha tajir na Masikini hakika lingekua Sawa
@@mosesnyelo1380 Kwa Nasaha za kibinadam hawezi kataa inakua ana Moyo wa kipekee. Me wazo langu viongozi wawajibike kwenye Sito faham kama hizi kwa Nasaha. Sio kufanya wanavyo fanya Mwisho wa siku kakutwa Mtaroni kafa, au raha Zao kuona Movie za Aina hizo
Huruma nayo ina garama, kubwa. Unawzakufanya huruma ikagharimu. Dar shida, kuna watu walifanya huruma hivyo tena wakashia kuendesha kesi kea miaka mingi, haki iko wazi. Iwe fundisho kwa tukuwaheshimu watu wasio na pesa.kama sisi. Ziara za makonda wale waliokatakata mtu vile ni akina nani. Siku akipatikana kiongozi wa kumpa haki. Tutaumia?
Uzuri ushasema mungu ni mungu wa haki na haki ya mtu haipotei. Hata mwenye hio nyumba anahaki yake pia kuna kesi nyengine za ardhi madudu yanakua ya baadhi ya watendaji wa ardhi wenyewe kwakutaka janja janja. Asa we kesi miaka 20 nyumba inavunywa leo huoni kuna sehemu kuna kosa hapo. Alijengaje kibali alipataje cha ujenzi? Nani alipitisha planning ya nyumba? Yani kuna vitu vingi hapo havikufatwa. Wanatakiwa watibu tatizo sio dalili za tatizo
Tunaimarisha uchumi, tunauboamoa tena dahhh, hapo kuna viongozi wa mitaa,mipango miji wanaona toka ujenzi unaanza, kwa nini wasiuzuie kama hakuna vibali vya ujenzi, ama kesi mahakamani?
Kwa mara ya kwanza nimeanza kuwa na imani na wizara ya ardhi nilikuwa sioni kabisa umuhimu wake ila awamu hii nimeanza kushawishika na utendaji wa wizara hii
Hili ni sehemu ndogo ktk kudhulumu haki za watu. Watanzania wasio na pesa wanadhulumiwa sana. Hii ni wizara zote za serikali. Mbali ya ardhi, tunataka mawazili wenye matendo, siyo kufanya maigizo. Wizaara zote mnaumiza watu.
Sasa Inakuwaje Mpka Watu Wanamiliki Ardhi Ambazo Sio Haki Yao..? Na Kwann Ww Kama Waziri Usipitie Hao Waliofanya Makosa Ndani Ya Wizara Mpka Uende Kuumiza Wasio Na Hatia
Ndani ya dhuluma hakuna haki..!..huyo na wengine waliopora viwanja vya watu wenye nyaraka halali lazma washughulikiwe..!..kesi ya KUGHUSHI itamuhusu na wenzie walioko Ardhi
Mheshimiwa Jerry silaha naomba uje Dodoma wilaya ya kongwa kata ya pandambili wananchi tuna kero nyingi sana, Kuna mtumishi anaitwa petronila shirima amekuwa na tabia ya kuvamia maeneo ya watu na serikali ya Kijiji ipo kimya tu, kiukweli tunaumia sana sisi masikini
Daaah kiukwel ni hatr ila mwenye aliyejenga nyumba angekubali kukaa na huyo mama amnunulie kiwanja kingine saw na hicho kuliko kula hasara ya ghoropha kuvunjwa jamn daaaah wangeelewana jamn yasingefik huko hata angemwongezea na hela kidg kuliko hvo hasara kubwa hvo kisa kudhulum