Allah awazidishie kheri na baraka baba kiruwasha na sheikh bachu mnawakilisha hekima katika jamii yetu. Binafsi nimependa hili suala lilivyohitimishwa, kwamba ni vyema kupima madhara na faida ya kumtumia jinni kabla ya kuchukua hatua hiyo. Asanteni sana kwa i'lmu.😊
Mm katika hili jambo nimemuelewa zaidi sheikh BACHU nasiamamia hapo. Kumtumia jini nirahisi zaidi kumtoa MTU ktk tawaqal kwa Allah na ndio njia rahisi yakuzama ktk shirki bila kujua au kwa kujua hasaaa Wallah aalam
Allah ukuhifadhi shekh huyo bachu anajua utafungua watu ukweli wataujua yeye kaja kujiweka ujuaji zaidi bila uchanganuz Kama hivo tukanufaika navyo rad hazijengi tunabomoa jaman tutumiane dhana mzur bila jazba kitu wanakijua hawataki kifahamike uzur
Wewe uliecoment kumtupia lawama bachu yakuwa amekuja kujifanya mjuaji sio kwei chukua kauliyake baba kuluwasha mimi natumia kitabu na yeye bachu sio manenoyake anatumia kitabu namwenyewe kasema amepata faida kubwa kwa bachu
Shekh Mohammed Bachu hajasema haifai kuwatumia lakini kuwatumia Kuna madhara mengi ... Na kitu hata kama kina maslah madhara yakiwa mengi kinaachwa maalim... Iwe tunatosheka na dalili... Na tumuelewe mtu kile anachokisema... Unarudia Yale aliyoyasema... Lakini je hujui hayo madhara Mzee wetu... والله المستعان
Hakuna aya wala hadithi inayoelezea kufanya hayo. Kwa nilivyoelewa kwamba kutunia majini wema kytafaa kwa dharura n sii iwe kawaida. Mtume swallahu alyhi wassllam ndio aliwasomesha na sio kuwatumia. Na ruhisa hiyo itabaki kwa maulamaa waliobobea elimu. Sio mashekhe wasasa wamitandaoni, Na hili jambo sio muhimu muhimu. Hebu watu wakasime yaliokiwa y muhimu yamejaa, tusikimbilie majini.
WAPIGA RAMLI IMEWATACHI SANA KUAMBIWA NI HARAM.. WALIKUWA WAMEJIFICHA LAKINI SAHII WANAJITOKEZA MMOJA MMOJA KUTETEA SHIRK ZAO... SHUKRAN SHEIKH MUHAMMAD BACHU
Njia ambazo hazina shaka hatuzifati kwa nini tulazimishe kwanjia zenye mashaka ??kwanini nauliza kwanini njia salama zipo hazina shaka hata kidogo lakini kwanini tutumie njia zenye mazonge kwann??
Ndg yetu Baba Kiliwasha kwanza muogope Allaah pili huna elimu ya kumjua huyu jini ni mwema au mbaya tatu ili jini akutumikie lazima pawepo badala ya kumpa jini na badala yenyewe haiwi ila ni jambo la haramu tuu nne maneno ya mwanachuoni yeyote sio qur an wala hadithi tunaweza tuukaachana nayo na hatupati dhambi
Nimegundua KITu bachu kwao wao Ibny Taymiya humfanya kama ni mtume na akitelezaa wao Shekh wao Huwa hawakubali kuwa kakosea Ibny Taymiya Kazungumzia kuhusu kasema ina faa lakini Wao kwao hawathibishi Wao wanapindisha maneno na kusema ya kwamba wao wanaangalia athar
Baba Kiriwasha ameelewa somo kutoka bachu, lakini nadhan shida ipo kwamba sisi binaadam wa sasa hatuna ubavu wa kumjua jini mwema 100% ili tutimize hiyo mubaha, Mitume ndio walikuwa na upeo huo, nashkuru kwamba masuala ya mapete ya bahati ya Dr Sule umemuachia mwenyewe Dr Sule umejiweka mbali na ushirikina, wewe umekuja na kitu mubaha tu, tumekuelewa
Wanaosababisha wanazuoni wakubwa kutukanwa ni nyinyi mashee musio waelewa sasa angalieni sana ila nais kilowasha ajamuelewa bachu au unataka tivii Yako watu watazame Kwan mada za ndoa umeishiwa shee
😅 aslam alekum akh mm nilivyo muelewa shekh bach ni kwamba yafaa kutumia majini wema kwa mamb ya kher ila tu ayo majini kuyatumia ninjia moja wapo wa kukupelekea ktk ushilikina
Kama kuwatumia Ni njia ya kuelekea ktk ushirikina vip ifae Tena kwanin isiwekwe Waz kuwa haifai kabisa kuepuka mashaka hayo Tung kwa hao mashekh wakubwa
Eti kuna mwanamke ana swahibu jinn Kitendo cha jinn kukaa ndani ya mwili wa mwanadamu tayari ameshakufuru Iblis ana njia nyingi sana za kumuingia mwanadamu ....
Haifai madhara mengi kwani jambo la msingi majin hatuwaoni hivyo itakua ngum kubaini nani mwema na nani anafanya khiana hivyo mambo yenye kutatiza ni vyema tukaachana nayo kama sheikh muhammad bacho asemavyo
Baba kiwasha kauli ya ulamaa ikiwa haina mashiko tunaiwacha tunashika dalili... وقال ابن أبي حاتم : حدثنا أبي ، حدثنا فروة بن المغراء الكندي ، حدثنا القاسم بن مالك - يعني المزني - عن عبد الرحمن بن إسحاق عن أبيه ، عن كردم بن أبي السائب الأنصاري قال : خرجت مع أبي من المدينة في حاجة ، وذلك أول ما ذكر رسول الله صلى الله عليه وسلم بمكة ، فآوانا المبيت إلى راعي غنم ، فلما انتصف الليل جاء ذئب فأخذ حملا من الغنم ، فوثب الراعي فقال : يا عامر الوادي ، جارك ، فنادى مناد لا نراه ، يقول : يا سرحان ، أرسله ، فأتى الحمل يشتد حتى دخل في الغنم لم تصبه كدمة . وأنزل الله تعالى على رسوله بمكة ( وأنه كان رجال من الإنس يعوذون برجال من الجن فزادوهم رهقا )
Wasiokua waislam tangu lini wakaridhika na uislam?Uache kuangalia uislam wako unasemaje we unakaz ya kuridhisha wasio waislam.Huu ndo mtihan wa kutumia akili kwenye dini pasina dalili.
Baba kiruasha unatetea sana au ndio mambo yako? Pamoja na hivyo hujatoa aya ya quraan wala hadithi umesoma maneno ya wanashuoni je unajua hao wanachuoni tunatakiwa kushikamana na maneno yao pindi wakiyaegemeza kwenye dalili ndio imamu maalik alisema: kila mtu kauliyake inachukuliwa na kuachwa ila mwenye kabuli hili, akiashiria kabuli la mtume swalallahu alayhi wasallam, Baba kiruwasha hayo mambo unayotetea utapoteza watu mche Allah imani za watu ni ndogo sana zama zetu mafsada ni makubwa kuliko faida ukija tena kutetea utoe na aya au hadithi kama huna funga domo lako
Mm nimekupenda shekh kwakukubali shekh bachu yale aliyoyasema simaneno yake bali nimaneno ya mashekh masha Allah nimekupenda bure mzee kwakukubali ukweli. ngoja tumsubiri bachu ajekumaliza kazi
Eti kuna mwanamke ana swahibu jinn Kitendo cha jinn kukaa ndani ya mwili wa mwanadamu tayari ameshakufuru Iblis ana njia nyingi sana za kumpoteza mwanadamu Allah atuongoze na kutupa mwisho Mwendo
Mimi pia najua hivyo.Kitendo cha jinn kukaa kwenye mwili wa mwanadamu anakuwa ameshakufuru. Lugha nyepesi ni kwamba hakuna jinn mwema anayefungamana na wanadamu,majini wema wote wanaishi ulimwengu wao wakimuabudu Allah S.A
Baba kiriwasha kumbe wale wanao tumia chuma ulete kumbe Ni jini. Subhana Allah ,,,, Yarrab tuhifadhi waja wako na utulinde na hasad na husda na vitimbi vya kiduniya. ,,, amiiiiiin
Yeyote anae amini kuwa kutumia jini inafaa basi huyo ni Mshirikina tu ikiwa binadamu tu yaliyojificha mioyoni mwao hatuyajui je itakuwaje kwa majini viumbe ambavyo hatuvioni? Huyo Baba Kiruwasha ni Mshirikina tu hana jipya.
Kutoka kwa Hafswa bint Omari bin Khattwabi- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayemuendea mpiga ramli akamuuliza kuhusu lolote, akamsadikisha, haitokubaliwa kwake swala yoyote siku arobaini". Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Mi nataka kusikia kasema HABIBY MUHAMMAD S.A.W .... sio mashekh ambao hata hadith za mtume wa allah haziwajui wanakazi ya kupoteza umma tu hamna lengine....
Arafu maneno ya shekhe matupu bila kuegemeza na dalili huwezi patia imamu shafi mwenyew alisema , ilipo aya ya quruani na hadithi ndo madhebu yangu yalipo mkiona maneno yanaenda patupu yatupeni mbali shikene dalili kwa mtume sasa ww mwenzio alisoma maneno akaegemeza na dalil ww wasoma matupu ya wanazuoni bila kuegemeza dalili
BAADHI ya Watanga wamelelewa kwenye familia zinawaganga matambiko , hivyo zikija mada zenye utata kama hizi zamajini lazima waziunge mkono.( Zingatia neno BAADHI)
Sheikh sijui ulifikiria unachoongea Unanasibisha MIJI NA AKILI HII INAONEKANA HUNA UELEWA TENA MCHACHE SANAH SIKILIZA SHEIKH ANATUMIA MANENO YA WANAZUONI SASA TANGA NA MAJINI YANAHUSIANA NINI SHEIKH DO YOU LISTEN TO YOURSELF
Mashaallaa Allah bariq mwenyenzi mungu akujaze maarifa zaidi na afya njema ili uzidi kutupa elimu, mwenye akili timamu amekuelewa na yule mbugila mbugila hatokuelewa kwa ubishi wa asili yake.
Assalam alykum sheikh baba kiruwasha mimi nimechelewa kuangalia haya maf-hum yako na pia nimeyaelewa vizur tu - tunanukuu maneno ya dr sule alisema inafaa kumtumia jini kwenye mambo ya mali (akuletee mali) katika fat-waah yako hujalizungumzia swala hili na mimi nahis swala hili ndio limeleta mtafaruku mkubwa katika jamii ya kiislam hivyo tunaomba ufafanuz wako kwenye hili pale tu utakapoona hii comment yangu,,Jee inafaa kumtumia jini kwenye mali (iwe kukuletee kwa namna unayoijua ama usioijua) wabillah tawfiq
Madhara ni mengi HAIFAI KABISA na baadhi ya wanaofanya hayo mambo hawajasoma dini vya kutosha. Tafadhalini sana huu mlango msiufungue ni fitina kubwa watu watapotea.
Alafu umejikita zaidi kwenye hukmu mubahu mubahu maulamaa wanasema itafaa kumtumia kwaajili ya da'awa kwa wenzie kwa vile tunaitakidi kwenye vikao vyetu vya kielimu wanakuepo sio kumtuma kwenye haja atakuludishia vipi majibu na yeye mpaka akae kwenye mwili wa mtu ndio aongee na huo ni uasi aruhisiwi kuingia mwilini kwa mtu
Point ya msingi kabisa..haya watatudishiaje majibu kuwa dawa imefika..kifupi hao viumbe wapo kwenye himaya nyingine tuu..abgalia kipindi mtume swallahalywasam alipoenda pamoja na yule swahaba alimcholea duara asitoke hapo.kisha mtume akaanza kuwasomea ...kwa ile khofu ya yule swahaba ilibakia akidogo atoke.na mtume akameambia raiti angejaribu kutoka njee ya hiyo sehem angeungua..sasa unasemaje kuwatumia hao viumbe kimchezo mchezo...mie nahisi ni kukataa tamaa kukubali uwezo wa mwenyezi mungu....au kama kipindi cha nabii suleiman kipindi alipo taka kile kiti cha malikia. Kuonyesha mwanadam ni bora aliketa kile kiti...kwahiyo wasiwape shavu hayo majini hakika hiko tuendako inaweza kua hatari zaidi
Tatizo ufaham wa watu ni mdogo.Elim uliotoa ni kubwa imezidi ufaham wao.Anaesema anataka qaala ALLAAH NA QAALAL RASUUL, ASOME AYA 2.Ya kwanza surah Albaqara Aya ya 29 .Yeye ndie aliekuumbieni vyote vilivyoko ktk ardh.Ukisema kitu ni haram we ndo unapaswa kuleta ushahid.Ngurue ni haram imetajwa kwenye quran, we unakula fenesi,mapera maparachich vimetajwa wap kwny quran.Waachieni wasomi mambo ya kielim.Quran ingeandika ugali, mlenda nk. Kitab tungekibeba na semi.Lakin zatumika kanun za aya kujua halal na haram.
15:16 kama amesema inafaa nae amekosea kuna.mambo mashekhe hawajui lakini sisi wengene tumeishi.katika familia.ambazo tunakuta wazee wanafanya mambo hatujui asli yake... mfano: kuna mda tunaogopa tusipo chinja kinaweza kutokea chochote... ndio hayo munayo ungia mkono... jini mwema yupo na mbaya yupo,,, lakini.hayo kwetu ni.Ghaib.... utasaidiana.na.jinii vile uthaimin alivyo elekeza lakini tujuwe jinn karne inaisha yeye bado ni kijana lakini wewe ushasahauliwa lakini kuna mitego alisha weka kuwakamata kizazi chako...
Sheikh unayumba na unawayumbisha wanao kufuatilia achana na mada hii iko mbali na upeo Sheikh wangu na sio aibu kutojua yote katika dini huna haja ya kuminyana masheikh pia wanakosea usishikilie ibun taymiyah tu yule ni mwanachuon mkubwa mchamungu mwenye elim kubwa lakini anaeeza kosea pia katika kauli zake au akaeleweka vibaya kwa wanao soma fatuwa zake kikubwa tujue haifai kutumia jini kwani allah ametutofautisha kimaumbile na kila kundi tunatakiwa kumuabudu Allah na sio kwa kazi hiyo wanayo fanya Washirkina, sheikh unataka kuziporomosha mada zako watu wa TAWHIID waache kuzisikiliza hebu achana nayo hayo turudishe kwenye mambo ya familia Tufaidike. Uko unako enda unaenda kutufanya tukatae na mada zako je mada zako zikipotezewa kwa tatizo lako ndio umepata faida.
Mtu ana kesi anadaiwa kweli anatumia jini kuharibu kesi..mty anataka mtoto wa watu amzini anatumia jini.mtu anataka kumdhuru mtu kwa dhulma anatumia jini...ndo hivi alikusudia sule...
MANHAJ SALAF NDIO MAPITO SAHIHI YA KUENDEA UISLAM WETU HUTOKAA KUSIKIA VITU VYA KITOTO KAMA HIVI KWENYE SOCIAL NETWORK. HUWA MAREJEO NI QURAN NA SUNNAH KWA UFAHAMU WA SALAF KINYUMECHO MTABURUZWA NA MAKANJANJA WA MJINI MPAKA BAAS
Msiba mkubwa na Africa umasikini tunao sana yaani watu kutukia majini na si technologia kisa dalali ktk mijitabu eti shekh ul Islam kasema ! na si Allah.
wanaokoment weng naon wanachochea ugomv tu kauli za maulamaa ndo zinachambuliwa nyie mngesikiliza msitumie nguvu ya hoja uyu sheh kuzungumzia ivo hainamaan ameunga mkon bali anazungumzia alichokiona
Mm naon uyu sheikh maskio yake ayaskie sisi tuna mfata mtu Muhammad sww ajiuliz kwanz km mtu Muhammad aliwatumie majini? Tujuw km ni suna ama ni faradh kutumia jini?
Na Sheikh uwe careful kwa maneno yako kwa sababu utajuzisha jambo na watu 'awaam watasema Shekh Kiruwasha amesema iko sawa..na watu wengi hawana hiyo elimu (na hata wewe Sheikh huna hiyo elimu) ya kujua jini gani ni Muislamu na yupi sio Muislamu.. sisi hapa duniani tunadanganywa na kuwa conned na watu tunaoishi nao hapa hapa duniani na tunawaona, je majini wenye hatuwaoni je? Sheikh Kiruwasha, tumche Mwenyezi mungu. Mtu asije akaingia kwa huo mtihani na siku ya Qiyama akakutaja kuwa alikusikia ukisema ni sawa kutumia majini.
@Abdullahhijma... Assalaam Alykum vip hali. Tatizo sio yy yeye kanukuu maneno ya wanachioni kama ni sehemu ya dalili ya hoja yake. Lamsingi Ni hili........... Mashehe wakae na kuangalia lile lisilokua na umuhimu, hata kama linadalili basi waliache na Wafanye kazi ya kulingania nasio kubisha.... أسلام عليكم ورحمة الله وبركاته
Sheikh Bachu kaeleza kiufasaha kabla hujajishulisha kumtumia jini unatazama faida na hasara zke ambapo akasema kutumia jini atakuplka ktk shirk moja kwa moja ajil ya maagano yko kati yake vilevile ao majini utawatambuaje kua uyu mwema na uyu mbaya ilhal hatuna uwezo wa mitume kuwatambua vyma.
@@jumaa052 huyo ni mtume wa Allah, Allah aliwaandaa mitume wake wawe vigezo na walimuabudu Allah kwa yaqini ya kweli wala hawakumshirikisha na chochote ktk viumbe wake.
@@jumaa052Nabii suleiman alipewa uwezo wa kuishi majini kabisa na kuwatumikisha ndo uwezo alipewa na pia mitume na manabii wana uwezo binafsi vp mm na ww mtihani sheikh iman zetu ndogo lazima tuingie kwenye shirk
Shekh wangu sikiliza vizuri Umeambiwa kutumia Majini kuna faida chache kuliko madhara, kama madhara n mengi shekh İbn Tamiyyah anamaliza kusema sio vizuri Kuacha ni HAULA zaidi 1- majini wabaya 2- majini wazıri lkn aina zote hiz wanakupelekea kwenye Ushirikina ! Sikiliza vizurii shekh nahic utaelewe vizuri biidhin kariimu
@@shawwalmsati3405ila baba Kirwasha katoa vitabu vi2 vya sheikh Uthaymin kimoja chakubali kutumia majini wema na kingine kinakataa kwa kuhofia mahsad yatakayotokea kwa kuwatumia majini. Tanbihi, ikiwa kichwa chako ni kizuri kufikiria basi yatosha kujiweka mbali katika kuwatumia viumbe hawa.
Mashallah, ilmu ni bahari, usilolijua ni sawa na usiku wa giza, nimekuelewa sana babu kiluwasha, nimemuelewa mohamedi bachu kila mmoja kwa anachojua yuko vizuri. Hizi ilmu zipo isipokuwa hatuzijui tuu. Allah atujalie elimu zenye manufaa fiduniya wal akhera
Ameen,hainahaja ya kubishana , kila mtu katika hawa ukiangalia kunakitu kimoja muhimu,wamekigusia, KAMA KUMTUMIA KWANJIA YA HALALI NA WASILA ITAKAYO TUMIKA KUMFIKIA YEYE BASI NI HALAL YAFAA, KAMA MAMBO NIYA HARAMU NA NJIA ITAKAYO TUMIKA NI YA HARAMU BASI NIHARAM,
Alafu wengi ktk watu wanaenda kulingana na fikra na akilizao, kwakuwa hajazowea hilo basi yye anaona hata sheria imekataza, Kwaivo mtu azingatie, kama madhara ni mengi kuliko faida kwake haifai kutumia, kama faida nyingi na njia atakayoitumia niya halal basi yajuzu, asiambiwe ni shirki
Sasa unapotumia jini mfano shekh sule alivyokua akisimulia mtu anakesi ya kufungwa bila kuonewa anatumwa jini kwenda mahakanani kuiba file vipi hapo sio dhulma hiyo.
Nimakosa makubwa sisi kuongelea na kujifananisha na Nabii wa Allah Suleiman yeye ni mfalme pia ni Mtume alikua pia anawasiliana na wanyama na viumbe wengine Malaika na Majini , sasa kwa hayo machache si sahihi kupigia mfano na kujilinga Nisha nae, Allah atupe ufahamu mwema.
Unatuchanganya ba ake ruwasha maana huyo jini anatakiwa azungumze na wewe ana kwa ana akikuingia mwilini tayari ni shiriki je wewe unakutana na hao wema ana kwa ana?
Baba kirwasha sjui ni nni unaongea tena maaana tumekusklza bado tu hatukuelewi ;mbon maelezo ymetolewa;majin unawatuma kw mambo yadaw kuwalingnia wanadam au majini wenzao ?je mpk uwatume wakiwa wapi maaan sjui. Unasem swahib sas yale wakirst husem mnafug majin ndo mambo km hay
Elim anayo Ila kudhania ndio kunaleta shida Kama ikiwa Kuna majini wema sifa ya wema kutenda hak vp uwadhanie kuwa wataleta shirik mbeleni au njia za kuwasiliana nap kuwa na hitlaf ? Kinachotawala Ni dhana ya ubaya Kama yafaa akaja kwa wema ukibadilika nawe mwache kaasi Kama mwanadamu tu
Mtume aliusia kwamba Wana wa Zuoni watakuja iharibu Dini/Watauharibu Uislamu na ndo hayo/ahaya yanayotokea Sasa (Ishara/Daluli) Mwisho wa Dunia umekaribia.. Mtume aliposema anawakhofia Wana wa Zuoni watakuja iharibu Dini, Mtume hakuwataja Kwa Majina yao hao Wana wa Zuoni na Wala hakutaja Maeneo/MaTaifa watakayotokea/walipo(Wanapoishi) hao Wana wa Zuoni ni Tz, Kenya, ZNZ, Saudia nk.🙌