Тёмный

KAMA UNATAKA KUFUGA NYATI MAJI 'MILANGO IKO WAZI NJOO UCHUKUWE MBEGU SERIKALINI' 

GSengo
Подписаться 51 тыс.
Просмотров 42 тыс.
50% 1

Shamba la Mifugo la Mabuki lililopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza lilianzishwa mnamo mwaka 1966 baada ya Uhuru wa Tanganyika kwa ajili ya kuzalisha F1, hii ilikuja baada ya kugundua kuwa wafugaji wachache waliopewa ng’ombe wa kisasa kutoka Ulaya, wengi wao walishindwa kuwamudu wakafa ndipo wataalamu wa Mifugo waliokuwepo enzi hizo wakaona ni vyema kuzalisha ng’ombe wa maziwa wanaoweza kuhimili mazingira ya nyanda za nchi zenye joto ikiwemo Tanzania.
Shuhudia ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina akizuru Shamba hilo la Mabuki kama sehemu ya mwendelezo wa Agenda ya Kitaifa ya Utafiti wa Mifugo, Uvuvi na Ukuzaji viumbe kwenye maji 2020 - 2025 ambapo pia amepata fursa ya kuwaona Nyati Maji wanaofugwa kituoni hapo, mbegu iliyoingizwa nchini enzi za utawala wa Rais wa Kwanza nchini Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere.
Kwa wale wanaotaka kufuga Nyati hao, kitambo sana Serikali ilishafungua milango.
TAFITI ZA AWALI.
Kwa tafiti za URT za Mwaka 2015, Tanzania inashika nafasi ya pili kwa wingi wa mifugo barani Afrika ikiwa na ng'ombe milioni 25, mbuzi milioni 16.7, kondoo milioni 8, nguruwe milioni 2.4, na kuku milioni 36.
Kati ya ng'ombe milioni 25 ng'ombe wa asili ni 98%. Hivyo, ni 2% tu ya ng'ombe wote Tanzania wanaofugwa kwa mfumo wa ufugaji wa kisasa.
Tafiti hizo zinaonesha kuwa ufugaji wa asili unachangia 7.4% ya pato la Taifa na ongezeko la ukuaji la 2.2% kila mwaka. Ufugaji wa asili umethibitika kiuchumi kuwa na ufanisi mkubwa katika matumizi ya ardhi na uhifadhi wa mazingira.
Ufugaji wa asili unategemewa na idadi kubwa ya Watanzania kwa kuendesha maisha yao; iwe kwa chakula, mavazi, na maendeleo kwa mapana yake.
Mchango wake katika uchumi rasmi na usio rasmi (informal and formal economies) ni dhahiri hasa kupitia kodi na tozo mbalimbali katika masoko ya mifugo, usafirishaji wa mifugo, ukaguzi wa mifugo, na upatikanaji wa malighafi kwa matumizi ya viwanda mbalimbali.

Опубликовано:

 

4 окт 2024

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 20   
@matukiosafaris6508
@matukiosafaris6508 3 года назад
Maelezo mazuri lakini kila ukipiga simu ili ununue ngombe unaambiwa hakuna
@frankjackson2784
@frankjackson2784 5 месяцев назад
Nimeipenda
@SimonShoo-mw8nk
@SimonShoo-mw8nk 2 месяца назад
Swali unango'mbe wangap Jibu tunaweza kuzalisha kadhaa sasa takwimu za ranch hamuna au???
@elisantemrita9894
@elisantemrita9894 3 года назад
Embu acheni siasa kwenye ufugaji Ongezeni akili katka ufugaji
@Nyanimzee
@Nyanimzee 2 месяца назад
Minataka ndapateje
@davidmsalilwa9687
@davidmsalilwa9687 2 года назад
Wanapatikana wapi
@amanibwire4423
@amanibwire4423 3 года назад
Pamoja na yote kama mfungaji nayeanza unapenda niwakumbushe kuwa ng'ombe wa kienyeji wana maziwa mazur na nyama nzr
@omarimnyeshani1810
@omarimnyeshani1810 4 года назад
Duuh!! Nyati tunao wengi tu mbugani halafu wataalamu mnaomba mbegu kutoka nje ya nchi? Hivi mnafeli wapi?
@avyalimanaathanassambuta6577
@avyalimanaathanassambuta6577 4 года назад
Nyati wanao tafutwa ni Domesticated
@TM.Sullusi
@TM.Sullusi 3 года назад
Usikariri mkuu, sio hao nyati wa mbugani kwetu. Ni aina tofauti kabisa ya nyati 😀😀😀😀😀
@matukiosafaris6508
@matukiosafaris6508 3 года назад
Kungekuwa na nyati wa mbugani hapo hao watu wote wangekuwa marehemu na wengine hospitali
@ndukulusudikucho_
@ndukulusudikucho_ 3 года назад
@@matukiosafaris6508 hahahahahaa
@mebumohammed6844
@mebumohammed6844 4 месяца назад
@@avyalimanaathanassambuta6577naweza pata number naitaji madume tu
@damasmaleo4845
@damasmaleo4845 2 года назад
Mbuzi mauza bei gani
@LemaliMeyasi-r4c
@LemaliMeyasi-r4c Месяц назад
Uko wap
@habibuluyangi2702
@habibuluyangi2702 Год назад
Mabuki iko mkoa gani na hao nyati maji bei gani
@filbertnashon7160
@filbertnashon7160 5 месяцев назад
Mabuki ni mwamza wilaya ya misungwi
@chuzilapweza6517
@chuzilapweza6517 5 месяцев назад
kwanini sasa wanajitangaza kipindi cha nane nane na matasha peke yake?
@husseinhussein9971
@husseinhussein9971 4 года назад
Hao nyati ndio wale wa India?
Далее
Nimejenga Majumba kwasababu ya Mifugo
6:34
Просмотров 21 тыс.
HA-HA-HA-HA 👫 #countryhumans
00:15
Просмотров 4,6 млн
这位大哥以后恐怕都不敢再插队了吧…
00:16
MAONESHO YA MIFUGO KIBIASHARA 2024
34:29
Просмотров 7 тыс.
MBUZI WA MAZIWA [ PART A ] || AKILI SHAMBANI
11:39
Просмотров 2,8 тыс.
Meet Uganda's biggest Goat Importer | Sinza Goat Farm
17:35
JINSI YA KUANZA UFUGAJI WA MBUZI | #MAVUNOTIMES
10:15