Kama watatokea watumishi wa mungu kama kumi tuu naiman Tanzania patakua mahali pazuri pa kuishi wahubili wengi ni wachumia tumbo tuu mungu akubariki sana na akulinde na wabaya wote na akujalie hekima zaidi
Wahubiri wengi sasa ni wahubiri kola tu, hawajui hata injili ni nini, mambo yanaenda kombo wao wanatafuna sadaka tu. Wewe Mbarikiwa ndio nakuona ni miongoni mwa wahubiri wachache sana walio tayari kutoa maisha yao kwa kutetea utu wa watu wengine. 1 Yoh 3:16, Katika hili tumelifahamu pendo, kama yeye alivyoutoa uhai wetu kwa ajili yetu, imetupasa na sisi tuutoe uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.
Amen na je nihalali kukashifu wengine nafikili pia kumtaja mtu pabric ainaya utakatifu ni uvumilivu ustahimivu ebullient soma mathayo 7 ,1 linganisha nahao unawataja pia matendo yayesu yalilitenga kanisa lamafarisayo kutokana na injiri waliyo ihubiri tumia nguvu hubris nene na siyo kuokoteza mambo yasiyo faa
Kuhubiri nikulitaja jina la Yesu, na wala sio mitume, someni na kuelewa mandiko, Injili ikija majina ya watu bila Kristo kujaa katika Injili iyo tunaona unatafuta kama watu wote wanavyo tafuta
Watumishi wengi hawapingi utekaji wala uonevu wala hawapingi dhuluma inayofanyika nchini wao wako Bize na kuuza mafuta na kukusanya pesa kwa waumini alafu wanajiita wachungaji sijui wanachunga nini. Uchangaji ni kuokoa na kuchunga, sio kujaza matumbo na kujilimbikizia mali, ( shame on them)
@@patrickmathiasnsalanga3401 Si kazi yenu kuwahukumu. Yaani unawapima watumishi Hao kwa jambo Hilo tu! Kwa hiyo umeipima kazi yao na kuona haifai! Nani amekupa uhalali huo! Unapofanya hivyo kumbuka 1Wakorintho 10:12, anayejidhania kuwa amesimama aangalie asianguke. Ukristo ni unyenyekevu ndugu yangu. Tena biblia inasema, Tusiwe kwazo la namna yoyote katika jambo lolote, ilitumishi wetu usilaumiwe (2 wakorintho 6:3). Kila Mtumishi atajibu mwenyewe mbele za Mungu. Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Kwa hiyo hata kama ipo sababu ya kumrekebisha mtu, na iwe kwa pole, si katika Hali ya kujihesabia haki na kuona wengine wote hawafai. Shalom!
Mzalendo wa kiroho na amani ,, ona Sasa wanawapa watu umaarufuu bila kujua,, changamoto ya akili kuhamiaa matumboni na matumbo kuhamia vichwani. God will stay and judge for justice.
Naomba nikuhulize mbarikiwa, kwani wew matendo mazuri wanayofanyaga hawa wakina magembe, abiud, na mwenginr unayajua mambo yao yote, au je unataka kila mtu akifanya mambo mazuri yote aseme na alete wahandishi wa habari.
Ndio inatakiwa yawe wazi kila mtu ayaone kwa sababu imeandikwa hivi katika Mathayo 5:16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Anakosea kulazmisha watu wawe kama yeye na haiji kutokea,hiv kukosoa au kuonya serkali ndo utakatifu? Mungu haoni kama yeye Wala mawazo yake si kama mungu anavo wawazia hawa anao wasema Kila sku
Hata kwenye CORONA MBARIKIWA Alinyoosha mapito ya bwana Yaani alidaka/alikuwa kama kichaka/aliongea Saana/kwamba yuko tayali kufa ila sio CORONA ijivinjari mitaani hilo alikataa kabisa alidema hayuko tayali kuona CORONA inakatiza mitaani ni ama corona ipoteee au yeye apotelee magelezani na kwa kudra za mwenyezi MUNGU TANZANIA ILING'ARA DUNIA NZIMA
Wacha MUNGU au Watumishi wa MUNGU ndio Pekee waliobeba Salama ya WATU/ndio wenye Majibu ya matatizo ya watu sasa wanavyokuwaga mstali wa nyuma kutetea watu sijuwi tuwaeleweje
Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha. [Warumi 14]
Kuokoka ni nini? Kwani unamwelewa Mbarikiwa? Kuokoka kutapimwa kwa mwenendo wa maisha kwa upendo na matendo ya mtu kumuelekea Mwenyezi Mungu. Bwana Yesu anasema "waniitaje Bwana na huyatendi nisemayo....? Pia "amri mpya nawapeni, pendaneni kama mimi nilivyowapenda..na amri kuu ni upendo!" Matendo yako ndicho kipimo katika utimilifu wa imani yako kwa Mwenyezi Mungu, si kupiga parapanda kama Mafarisayo, huo ni inafiki! Bwana Boniface ni Msabato (SDA)!
Watu wengi wanaojifanya ni watumishi wa Mungu makanisani na misikitini wako kwajili ya maslahi ya sadaka tu lakini mioyoni mwao hawana huruma hata chembe ni mashetwani wakubwa
Mimi ninachojua kila mtu amewekwa kwa kusudi. Jacob amewekwa kwa kusudi hilo, wewe umewekwa kwa kusudi hilo, akina Abiudi wamewekwa kwa kusudi lao hivyo usimhukumu mtu kama hajafanya kitu landa hajasikia hicho moyoni. Fanya wewe uliyekusikia.
Kunawakati unaongea sawa lakini unakosea unapokuwa unahukumu watumishi wa Mungu kanakwamba wewe ni mtakatifu ACHA kuhukumu wenzako muhukumu ni mumojatu wewe kazi nikuomba lehema na Toba tu napo nyanyasa na kuzalilisha waumini wako ndipo uko sawa je ukipewa uongoze watu 200 tu siitakuwa tabu
Nadhani nyuma yake wapo zaidi yake wanakuja, sidhani kama uo muda utafika... Mitume waliuwawa ila walizidi kuongezeka walio amini neno na kulishika sawa sawa zaidi... just wait
Neno Nabii na Mtume tunalitumia vibaya!! Hatuna Nabii wala Mtume Tanzania ambao wanaweza kututabiria kesho yetu, majira fulani na mahala fulani kutatokea nini. Ni wahubiri wanaotumia fursa za changamoto zetu za maisha tu na wala si wafariji kiroho!
Kamwe Watu hawatafanana maana biblia Iko waz Kuna MWENYE kuonya,MWENYE kutabir,MWENYE kufundisha Bali ROHO ni yeye yule kwahiyo kama wewe umepewa kutabir hi Uwez kulazmisha watu wote wawe kama wewe ,,KILA MTU ASIMAME MAHALI PAKE ILI KAZI IENDELEE KWA MAANA KILA MTU ATADAIWA ALICHO PEWA , WOTE MKI FANANA KAZI YA MUNGU HAIWEZI KWENDA
@@Mbarikiwa_Mwakipesile tasfr ya mwanadamu lakn mawazo ya MUNGU s kama ya kwetu , wanadamu kama ni hivyo tungeona aliyo Fanya Eliya na wengne wote wangefanya,aliyo Fanya Petro na Yeremia na wengne wengi.
hujui hata utakatifu ni Nini unaongea kipumbavu. Kañisa la MUNGU unaità misukule? Boni kamuokoa nàni kwa kipi? Tatizo la kutekwa utalimaliza kwa kukaa hapo na camera ukitafuta Kiki? Unalazimisha watu WOTE wawe Kama wewe? Nyie pambaneni kivyen7
Shida iko wapi! Ukitaka kujenga hoja jipe nafasi ya uvumilivu katika kumsikiliza mtu hata kama upendezwi na kauli yake. Wewe unaelewaje maana ya kanisa mpaka umuhukumu Mbarikiwa kwamba anaongea upumbavu? Boniface Jacob kamwokoa nani? Kwani kwako kuokoa ni nini? Basi, Boniface amewakatia rufani wafungwa kumi walioko jela kwa uonevu kwa kutoa fedha zake kuwalipa mawakili waweze kuwatetea wafungwa hao mahakamani. Pia ameahidi kufungua ofisi ya wanaohitaji huduma za kisheria kwa wale wasio na uwezo wa kuweka mawakili. Je, tukikiri kwamba katenda jambo jema ni dhambi mpaka utuone wapumbavu?