Kwaya Katoliki - Nitume Mimi Bwana (Na Frt. Godfrey Masokola)
Lyrics:
Verse 1:
Eee Mungu naitika wito wako, Umenijua mimi hata kabla sijaumbwa _Kabla sijazaliwa mimi wewe uliinitakasa
Bwana, toka tumboni mwa Mamangu Ukanifanya kuwa nabii na mtumishi Wako Niko tayari Ee Mungu.
Chorus:
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
Verse 2:
Unitie nguvu na ushupavu nisimamie ukweli Na kutetea Imani tena niimarishe Mimi nihubiri neno lako.
Mimi,ni mtumishi wa Bwana na Nitendewe ulivyonena na naja kufanya Mapenzi yako niko tayari Ee Mungu.
Chorus:
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
Verse 3:
Nijaalie Roho Mtakatifu aniongoze katika utume Wangu ili nidumu daima milele katika kukutumikia.
Bwana, nitume mimi kutangaza mwaka Wa Bwana kuwahubiri masikini Habari Njema niko tayari Ee Mungu
Chorus:
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
Nitumie mimi Bwana X 4
Naitika wito wako naja bwana unitume X2
___________END___________
nitume bwana
Nitume mimi Bwana
Nyimbo za upadrisho
28 сен 2024