Nakumbuka niliupata wimbo huu June 2023 “UMEKUWA MWINGI”
Wakati huo nilikuwa napitia mambo mengi mno ya kuumiza moyo na ku dhohofisha nafsi
Lakini kila nilipokuwa nikitaka kukata tamaa nilizikumbuka rehema na fadhili zake zilivyo kuwa nyingi kwangu na maisha yangu kwa ujumla kama Miriam Lukindo Mauki kama inavyo sema katika kitabu hichi
Psalms 40:5
BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu;
Hakuna awezaye kufananishwa nawe;
Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.
Na wakati huo pia , Baba yangu mzazi alikuwa hospitali akifanyiwa operation iliyokuwa sensitive, na katika mwezi huo huo tulikuwa tumemzika Shangazi yangu ambaye ndiye aliye mwachia ziwa Baba yangu. #MiriamLukindo #UmekuwaMwingi
18 сен 2024