Ni moja kati ya mahojiano ambayo natamani kuangalia kila iitwapo leo. Vizur saaana Mkasi, hongera kwa mahojiano na hongera kwa majibu ambayo yanaeleweka.
Swala la Watanzania nje ya nchi linatakiwa litiliwe umakini. Ila ni wakati wa nchi za Afrika mashariki kujivunia Undugu pamoja na Lugha yao ya Kiswahili kwa pamoja. Sanaa ya Tanzania inatumiwa na kutangazwa kama ya Mataifa mengine kama si ya Ulaya yenyewe basi hata ya nchi nyingine za Afrika.
Swala la uamuzi linatakiwa liwe la pamoja na si kama la mfano wa panya wanaotaka kumfunga kamba Paka na akitokea basi panya hujikuta wapo kila mmoja mahala pake. Umoja ni Nguvu, tujihadhari na mikataba isiyoeleweka , msanii anaweza kurekebisha mkataba kabla ya kazi,mf kipengele cha Kujitambulisha utaifa wake ni muhimu.
Tunaelewa kuwa wasanii wengi wanaandika mikataba kwa ajili ya kujikimu na mahitaji yao ya maisha kutokana na hali ngumu ya maisha,ila Haipendezi kuona nyimbo za kizaramo zinaimbwa na Wazimbabwe tena kwa kiswahili cha kubabaisha na kutangazwa ni za kizimbabwe.
Kumekuwa na taratibu za kuwaleta baadhi ya wasanii kufundisha tamaduni zetu na pindi wanapoondoka huwa zinarekodiwa na kutumiwa vibaya kwa lengo la kumgandamiza msanii wa Kitanzania.
WABONGO BANA KWA UMBEA ETI KIDUMU ANAJICHUA,NJOENI HOLLAND MUONE WANAUME KWA WANAUME WANAOWANA,ALFU NYOSHI S ALIKUJA HAPO MBONA UJAMUULIZA KUHUSU MKOLOGO,ACHENI ZUNU