NA WILLIUM PAUL, SAME.
WATUMISHI wa Umma wametakiwa kuhakikisha wanasimamia kwa umakini fedha ambazo zinaletwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kudai kuwa Chama cha Mapinduzi na Serikali hakitamvumilia mtu yeyote atakayetumia fedha hizo vibaya.
Kauli hiyo imetolewa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (MNEC) kupitia mkoa wa Kilimanjaro, Seleman Mfinanga wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa wajumbe wa Kamati ya Siasa mkoa wa Kilimanjaro wilayani Same.
29 сен 2024