Mkazi wa Ngerengere kaskazini wilayani Morogoro Hussein Steven (35) amefariki dunia kwa kuchomwa kisu sehemu za mwili wake na Kulwa Bosco wakati wakigombea shilingi mia mbili ,fedha waliyokubaliana kwenye mchezo wa Kamari
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa moja usiku katika baa ya Itonyaje maarufu Kama Maokoto katika kitongoji cha Ngerengere Kaskazini wilayani Morogoro ambapo marehemu alikuwa akicheza michezo wa kamari na mtuhumiwa Kulwa Busco na kuahidiana atakayeshinda atampa mwenzake fedha lakini baadae katika mabishano ndipo mtuhumiwa akamchoma kisu kilichopelekea kifo kwa Husein Steven na kwamba mtuhumiwa tayari anashikilkwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.
8 окт 2024