Watch KTN Streaming LIVE from Kenya 24/7 on www.ktnkenya.tv
Makubaliano yanayodaiwa yameafikiwa kati ya chama cha wiper na ODM, yamepata pigo kubwa hii leo, baada ya makamu wa rais kuyapuuzilia mbali. Musyoka ambaye alikuwa nje ya nchi, wakati makubaliano hayo yanadaiwa kuafikiwa, amepasua mbarika akisema wanaodai ameridhia kuwa mgombea mwenza wa waziri mkuu Raila Odinga wanawahadaa wakenya. Ilidaiwa kuwa odm na wiper watafanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa tononoka mjini Mombasa kuunadi muungano wao hapo kesho. Na huko Kapkatet diplomasia ya kupata baraka za jamii ya wakalenjin ilioendeshwa na kinara wa urp william ruto ilifika kileleni.
11 окт 2024