Wakimbiza wenge wa Uhuru mwaka 2022 wakiongozwa na Sahihi Geraruma wameonesha kutoridhishwa na gharama zilizotumika kujenga ofisi ya mradi wa maji uliopo katika kijiji cha Itete njiwa wilayani Malinyi mkoani Morogoro.
Baada ya kutembelea mradi huo na wamepewa taarifa ya ujenzi wa mradi huo ambayo pia ilibainisha kuwa ujenzi wa ofisi hiyo (Pump House) umegharimu Shilingi milioni 13 jambo ambalo hawakukubaliana nalo.
Mradi huo una vituo vya kuchotea maji 5, kati ya hivyo 2 vimekamilika na vinatoa huduma, Kwa sasa kazi ya ujenzi wa tenki inaendelea
Kwa upande wake mkandarasi Ramadan Mwerere anayetekeleza mradi huo alisema gharama hizo zinajumuisha jengo,umeme pamoja na Uzio unaozunguka jengo hilo, majibu ambayo hayakukubalika na wakimbiza mwenge hao.
Hadi sasa bado hakuna fedha iliyolipwa, Mkandarasi huyo atalipwa tathmini ikifanyika, atalipwa kulingana na thamani ya kazi itakayotathminiwa
Aidha mradi huo unaogharimu millioni 364.3 bila VAT kwa kutumia fedha za NWF. baada ya kukaguliwa na viongozi hao walikubali kuweka jiwe la msingi na kuelekeza kufanyiwa kazi marekebisho yaliyopo pamoja na kuongeza kasi ya utekelezaji wa mkataba.
#WasafiDigital
WATCH WASAFI TV📺
AZAM - 411 | DSTV - 296 | ZUKU - 028 | STAR TIMES - 444 & 333 | COCONUT TV - 20 | DODOMA CABLE - 113
LISTEN WASAFI FM 📻
88.9 DAR/ZNZ/PWANI 📻 | 104.1 DODOMA 📻 | 94.5 ARUSHA 📻 | 97.3 MBEYA 📻 | 94.9 MWANZA 📻 | SHINYANGA 106.3 📻 | KIGOMA 101.7 📻
Follow Us On:
INSTAGRAM: / wasafitv || / wasafifm
TWITTER: / wasafitv || / wasafifm
FACEBOOK: / wasafitv
𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 ©2021 𝑾𝒂𝒔𝒂𝒇𝒊 𝑴𝒆𝒅𝒊𝒂. 𝑨𝒍𝒍 𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕𝒔 𝒓𝒆𝒔𝒆𝒓𝒗𝒆𝒅.
#wasafi #wasafitv #wasafifm
5 окт 2024