Taylor Swift amekua mwanamuziki wa kike tajiri zaidi duniani, akimpita Rihanna na kuwa na thamani ya utajiri wa dola bilioni1.6. Mafanikio haya yanatokana kwa kiasi kikubwa na ziara yake ya “Eras Tour” na umaarufu wa nyimbo zake.
Mwanamuziki huyu ni wa moja kati ya wasanii muhimu pekee kwenye kiwanda cha muziki, kwani amepata utajiri huu wa kiwango cha mamilioni ya dola kwa kutegemea zaidi rekodi zake na shoo zake za live.
Ingawa utajiri wa Rihanna ulikuwa juu kwenye kipindi fulani, Taylor Swift sasa anashika nafasi ya pili kwa utajiri kwenye orodha ya wanamuziki wote, akimfuatia Jay-Z.
Mafanikio ya Taylor Swift yanaonyesha jinsi muziki unavyoweza kuwa na matokeo chanya kiuchumi, na kumfanya mtu kuwa mfano wa kuigwa.
🖊 @bboyrama_
POWERED BY @wizy_bracelets
10 окт 2024