Kwa hiyo uongozi wako ni bora kulko uhai wa mtu??..yani wewe hufai kuwa kiongozi,.na mtu akipotea utafutwe wewe nawe uwawe na wananchi!..we ni mchumia tumbo huna lolote wala uzalendo huna!
Sasa kwa kauli hizi za viongozi wa CCM kwanini watu wasife bila hatia. Kiufupi mnajenga chuki kubwa ndani ya nchi yetu. Maana mtu akiwa na chuki na mtu atasingiziwa kuwa amemtukana raisi ili auawe. Mungu yupo.
Hawa ndio watu wasiojuilikana leo wanaanza kudhihirisha maovu yao ya siku nyingi na hawa ndio wachochezi wakubwa wanaolindwa na jeshi la polisi laiti lugha kama hiyo ingeongelewa na mpinzani lahaula mapolisiccm yangekuwa yamefungulia kesi ya uhaini na dhamana hakuna
Shida ya ujinga kama huu ni system zipizotengenezwa kutoka juu kuwa bila uchawa huwezi kuishi kwenye uongozi imetuasili hadi vijana ndiyo maana wanajikuta wanaharbu Kwa kuongea ujinga
Ila ingekuwa ni Chadema,hapo ungewasikia polisi imepata taarifa za kiintelejensia wanataka kufanya vurugu.Lakini husikii intelejensia ya polisi ikifanya kazi kwa chama chao pendwa cha CCM.Ewe Mwenyezi Mungu tupitishe salama katika kikombe hiki,yaani mtu anajitapa hadharani kupoteza watu halafu watu wanamshadadia tu.Kana kwamba anaongea kauli nzuri.Hata kutaka sifa na kulinda vyeo sio kwa kutoa kauli hizi.Kumbukeni duniani tunapita,usiwanenee mabaya binadamu wenzio kisa kutaka sifa na kujikomba kwa wakubwa zako.
Ni vema kuheshimu sheria ya makosa ya mtandao sisi wananchi tunapinga upotezaji wa watu. ni matumizi mabaya ya Madaraka hatutaki siasa za vitisho kwanza mama Samia hautaki hayo mambo vijana acheni sifa
Eti, gharama ya Mungu kutuumba kwao ni ndogo sana, kiasi diwani wao apite kwa kutuua, na kuua watoto wadogo na albino kwa ushirikina, mbunge ashinde? Kwa mabao ya mkono, na kwa haramu na nusu haramu? Kwa kutunyima KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI?
Nikweli sio vizuri kumtukana mtu yeyote, ila huyo jamaa inabidi akamatwe kwa hiyo kauli yake kwamba atapoteza watu, hiyo kauli itachafua chama kwamba ndio kinapoteza watu.
Mimi nauliza, na wale Mawaziri waliotajwa na Makonda nao watapotezwa, au ni wanainchi tuu wasio na walinzi, Allah tuhukumie kabla waja wako hawajakutwa na mauti haya, viumbe wako hawana hofu na wewe tena