Haya mlikuwa mnayajua znz nzima kodi zinazohusu makusanyo ya sehemu za historical zinaenda serikalini lkn makusanyo ya mkunazini yanaenda kanisa la anglican nandio zinazowasababisha wagombane kwasababu hela ni nyingi
Huna sifa na umekosa sifa kweli yakuwa Askofu kwa sababu ya kauli zako harafu pia umesema unaishi America na huku Jimbo la Zanzibar linatizamwa na nani?
Huu ni ujumbe mzito wa kuzingatiwa na Viongozi wa Jimbo Anglican sasa basi. Askofu Mndolwa atafute Watu wengine NJE ya Maaskofu wa nyumba ya Maaskofu. Wapo retired bishops na Makasisi wastaafu Wakristo Watu wenye busara. Uongozi huu wa Jimbo umevuruga, umoja na historia ya Kanisa la Anglican lenye asili ya UMCA na USPG. Inatosha
Hawa Wakristo wa Zanzibar ndio pekee ambao baadhi yao ni nusu waarabu wenye asili ya Oman wamechanganya na waafrika, ambao kiasili hawakuwa Wakristo kama wale waarabu kama wazungu weupe wa Lebanon, lakini walikuwa Waislamu lakini waingereza wakawaingiza kwenye Ukristo wakati wanatawala Zanzibar na waliingia hivyo kama vile Agustino Ramadhani, na Wakristo hawa wa Zanzibar wengi ni wafuasi wa Kanisa la Anglikana
Kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad s.a.w na kuja kwa Uislamu, waarabu walikuwa kama tulivyosoma katika historia ya Uislamu, kwamba walikuwa aidha Wayahudi, wengine Wakristo lakini wale wa zamani wengi wao yaani Orthodox na waabudu masanamu kama wale kabila la Mtume wakiitwa Quraysh lakini baadae Mtume s.a.w alifanya kazi na waarabu wengi wakawa waislamu lakini wakabaki baadhi Wayahudi na Wakristo
Mtume Muhammad s.a.w alipokaribia kufariki akasema : Muwaondoe Wayahudi na Wakristo katika bara la kiarabu (yaani jazirah ya kiarabu yaani arabuni kwenyewe, yaani Saudia Arabia), hivyo zama za Khalifa Umar r.a, alipotawala, akatekeleza amri hio ili ibaki Saudia Arabia kwenye himaya ya Uislamu, hivyo alipoteka Lebanon na Syria, akaamrisha Wakristo waarabu wa Saudia Arabia wapelekwe kule wakahamishwe huku wale watu wa Lebanon na Syria waliosilimu waje Saudia Arabia na Yemen, na wakija Saudia na Yemen wachukue majumba ya wale Wayahadi na Wakristo na wale Wayahudi na Wakristo wa Saudia na Yemen wakachukue majumba ya wale waliokuwa Lebanon na Syria, na hivyo yakahamia makabila ya Kikristo ya kiarabu kama vile Bani Qahtan, Bani Ghassan kule Lebanon na Syria