Karibu kwenye Chaneli yetu ya Injili Milele, mahali tunaposhiriki ujumbe wa matumaini na wa kutia moyo kutoka katika neno la Mungu ili kukusaidia kukua katika imani yako na kuimarisha uhusiano wako na Mungu. Timu yetu imejitoa kutengeneza maudhui makini ambayo yatakupa changamoto ya kuitathimini tena imani yako na kukutia moyo katika safari yako ya imani. Tunaamini Neno la Mungu li hai na lina nguvu, na tunaamini mahubiri na mafundisho haya, si kwamba yatakutia tu moyo, bali pia yatakutayarisha kuishi maisha ya umilele. Uwe ni mtu uliyeishi maisha yako yote kama mkristo au mtu anayeendelea kuichunguza imani ya Kikristo, tunakualika kuungana nasi katika safari hii nzuri na ya kushangaza, ili kwa pamoja tugundue zaidi juu ya upendo wa Mungu na neema Yake kwetu.