~Mwalimu tajika wa somo la Kiswahili. ~Mfafanuzi na mchambuzi wa kazi za fasihi ~Mwelekezi na mshauri wa wasomi kuhusu maswala ya elimu ~ Wasiliana nami kwenye nambari 0707 286 397
Video ya 1 au msururu wa kwanza, maswali ya (a) hadi (f) ndio hii 👇 ru-vid.com/video/%D0%B2%D0%B8%D0%B4%D0%B5%D0%BE-V9hNSjSqMxI.htmlsi=h6Od6xUqQYRcqHbE
Kanzi kuntu mwalimu ❤....tumenufaika sana na kipindi chako hichi..... mwalimu tafadhali angazia Ufupisho na kudurusu maswali kwa karatasi ya pili kabla ya mtihani mwaka huu
Shukran sufufu 🤗, bila Shaka nitaangazia kazi hiyo kwa juma hili tu. Nitatumia karatasi za mwigo za shule za kitaifa kama Kapsabet, Mang'u, Nairobi, Pangani, Loreto Limuru na shule nyinginezo.
@@MwalimuWanjala siyo silabi nne kweli? maana sithani kama kwenye kiswahili tuna silabi yenye muundo wa KIK , aidha kama zipo naomba mifano zaidi tafadhali
1.Sara anakumbuka namna alivyopewa masomo ya unyago na nyanyake namna ya ya kuisha maisha ndani ya ndoa. 2. Yona anakumbuka akiwa miongoni mwa vijana wa kwanza kijijini mwao kuingia kwa dini. 3. Yona anahadithia wazee wenzake wa kijiji, Luka na Beni namna alivyokuwa akirauka mapema shuleni. 4. Yona anaambia wazee wenzake kwenye kikao kuwa hizo enzi akiwa mwalimu viboko viliruhusiwa. Yeye binafsi hakuwahi kukosa kiboko mkononi. 5. Yona anasema babake Kalasinga alikuwa mwafrika wa kwanza kuajiriwa na mhindi na kufanya kazi na kupandishwa cheo hadi akawa dereva. 6. Neema anakumbuka namna Yona alivyokuwa mkali, kuwagombeza na kuwapiga. 7. Sara anaambia Asna kuwa aliachia masomo kwa darasa la Saba kwa sababu enzi zao katika jamii Yao elimu ya mtoto wa kike ilifanyiwa bezo. Akishabaleghe aliozwa kwa lazima. 8. Kiwa anaambia Dina namna Neema walivyokuwa kama ncha ya sindano masomoni na pia akiangalia mtu usoni ungeona akizisoma fikra zake. 9. Sara na Dina wanasema kuwa kuna mabadiliko upande wa usafiri, kitambo wangechukua siku nyingi kufika mjini. 10. Bunju anapogorofishana na Neema , anamkumbusha mahali alimpata kwa ajali mbaya na kumuitia flying doctors na kusimamia gharama ya hospitali . 11. Bella anaambia Neema kuwa kitambo Mila zilifwatwa kwa Sana. Sasa hivi mambo ya mila yamepitwa na wakati. Sara anaweza lala kwa Bunju.
2. Wakati Dina ako kwa Sara, mazungumzo yananoga na kuingia kwa vicheko hadi wanasahau kuwa maji yameshachemka. 3. Bella na Neema ni rafiki wa dhati. Urafiki huu unamfanya wanasikizana na Bella anakaa kwa Neema kwa muda mrefu hadi Watoto wake wanamsahau. 4. Beni, Yona na Luka ni marafiki. Kila siku wanakutana katika kikao cha wazee wakijadiliana mambo ya jamii, mavuno na kuburudika kwa ujumla.