Ni mwaka 2004-2005 mkali wa rhymes competition sio 2006. Pia huyo dada arekebishe kidogo kauli mtu kama Afande, Prof Jay au Jay Moe hawawezi kutafsiriwa kama wanawaogopa akina Young lunya na wenzie kwa kutosikiliza nyimbo zao. Naomba nieleweke, no disrespect kwa vijana (Lunya na wenzie) ila wanachoimba kwa asilimia kubwa ni majigambo kila mmoja ni mkali kuliko wenzie ktk nguzo za Hip-Hop hiyo ni sehemu tu ya moja ya zile tano. Hawa wakubwa kutowasikiliza pengine ingefaa itafsiriwe kama challenge kwa vijana kuongeza juhudi ili kusikilizwa na jamii yote maana sio wasanii wakubwa tu wasiosikiliza kizazi hichi bali hata mashabiki wengi aged kuanzia 28 na kuendelea wengi hawasikilizi rap songs za sasa ukiwakuta na moments za music wanaenjoy Ile Ile miziki ya akina AY, Solo thang Juma nature na akina inspector na wengine. You guys ni wadau muhimu kwenye tasnia mnahusika Moja kwa Moja either kujenga au kubomoa heshma na nidhamu ya tasnia maana jamii inayosikiliza haina chaguo mkiwachagulia trash wataenda na trash mkiwachagulia conscious wataenda na conscious vyema kuchunga kauli zetu you're the bridge between artists and fans