Aibu kubwa sana kwa tamko kama hili.Viongozi wakubwa wanaoaminiwa na waumini wao kuruhusu jambo kama hilo ambalo hata mwenyenzi Mungu amelilaani katika kitabu kitakatifu. Ila kwa vile amelitamka yeye ,basi ni wajibu wa kila mtu anayeguzwa nalo ajifikirie yeye mwenyewe.Maana Mungu hakukosea kumpa mtu kuwa na kichwa chake peke yake kutafakari mabaya na mazuri yanayompendeza Mungu. Aliyetamka hivyo ni binadamu kama binadamu mwingine. Kwa hiyo anayetaka kuyafuata afuate ila ana kichwa chake cha kufikiri baya na zuri linalompendeza Mungu
Sisi wawata hatutaki watoto wetu kuwa mashoga tunafuata misimamo yetu ya kanisa katoliki wazungu wanatengenexa madawa ya kuwafanya watoto wetu kuwa mashoga ili wawapunguzie urefu wamaisha na kuwa bila watoto wakati Mungu alisema zaaeni mwongezeke mkaijaze nchi. Na mtumishi wetu askofu ni mwana wechu tunampenda sana anamaono. Ya kibiblia.
Tunasubiria Tamko la TEC, haya ya akina Ruwaichi ni janja janja! Kubariki wenye mahusiano ya jinsi moja ni kubariki ndoa zao, wasijaribu kujificha kwenye kichaka cha mchicha!!😊😊
Waache wafirani,sisi tupo tunataka tuwaone wanaenda mbingu kwa baba. Kama yesu angekuwepo nadhani angezimia kwa hiyo mineno wanayoiamua huko Vatican dah
Wewe mchungaji achana nakanisakatoliki papa si kanisa katoliki wala hatutaki kuhamia kwako kumbuka uhuru wanchi ulitokana na romani katolili. Kanisa hili ndiyo mmiliki wa yote
Mtangazaji una uwezo mkubwa sana wa kuelewa tamko la baba mtakafifu hata vibaka wana haki ya kupata baraka waraka unapinga kabisa ndoa za jinsia moja well done
@@saidbakar-qo6ri mbona na wewe unaendele na dhambi zako ila una hitaji Baraka. Je huna utofauti na mashoga dhambi zao?. Kwasababu dhambi n dhambi. Cha msingi tuwasaidie kiroho na sio kuwakashifu vibaya kama dhambi zao n kubwa kuliko ya kwako. Kama ww n mtakatifu endelea kuwakashifu
Hapa Mimi naunga mkono hoja, maana wanatuletea siasa kwenye dini,bora wajiuzulu ili tujue hawajaunga mkono hoja maana Kila mmoja anafafanua kivyake kwa hivyo watoe tamko la kiujumla
Hata kwenye bandari wakatoliki walipingwa sana kwa madai kwamba eti ili wapitishe mizigo bure bandarini...mmeona matokeo chanya basi mmepata reference...hata kwenye hili suala la ushoga ipo siku litafanyiwa reference chanya....
Huu mjadala ufungwe ushoga ni dhambi hakuna ubishi na ni vyema watu wakaacha ubishi na kufikiri. Hivi ukweli wa hiyo sodoma na gomora haueleweki kwani???
Tupo duniani kuna mambo mengi yanayoendeshwa na utawala wa shetani kiroho na kimwili na yesu alisema nakumtaja shetani ndie mungu wa dunia hii yeye kamshinda nawala hana kitu kwake mtu yoyote ambae hana imani ya Mungu wa kweli hawezi kumshinda shetani hata awe kiongozi mkubwa wa dini yoyote wenye Mungu wa kweli ndani ya mioyo yao na wenye imani ya kweli ktk kristo yesu waliotubu dhambi zao nakuziacha nakuishi maisha matakatifu yanayompendeza Mungu ndio pekee wanaweza kumshinda shetani nakukataa nakupinga mambo ya ushoga bila woga
Papa alikuwa na maana wawape baraka za maisha mengine siyo ya ushoga wao ndiyo maana alisema wasibaguliwe wapenzi wa jinsia moja ni dhambi kama dhambi zingine papa alivyo sema muwabariki siyo kwa ushoga wao bali kwa maisha mengine ya hapa duniani.
Kwisha kwisha kwisha ili si kanisa aliloliacha yesu wanachulia yesu kienyeji sana .nikanisa liligalim maisha ya watu mitume walichinjwa walichomwa waliliwa na wanyama wakark leo katoliki wanachaua ukristo oooo nalaaaani sana
Kuna sentensi moja aliyoisema Papa kwamba, "jambo lolote linalokwenda kinyume na Maadili ya Kimungu, haliwezi kubarikiwa". Kwa nini hiyo sentensi hamuisemei? Kwa nini mnachukua kamstari kamoja tu na kuacha mengi zaidi aliyoyasema Papa?
Nchi haikubaliani mbona wakati Museveni anapitisha sheria ya kupinga mahusiano ya jinsia moja mbona huyu wa kwetu yeye hakutoa tamko lolote zaidi ya kuendelea kutafuta misaada na mikopo! Hatutataki uchafu huo katika Taifa letu.
😂😂😂😂 I think it's better to proud your self if you believe in God and not prodding of being in any religious group since kitakachokupoleka mbingun sio dini yako isipokuwa iman yako kwa kile unachokiamini kuhusu Mungu wako.
@@lymondmande4422 Huo sio Ufahamu wa UISLAMU .. Hakuna salama huko tunapokwenda isipokuwa Kumuamini Allah na kukiri kuwa Muhammad ni mwisho wa mitume na manabii kisha ukatenda matendo mema na kujiepusha na maovu .. Kwa mujibu wa Imani yangu, hivi ndivyo salama ya mwanadamu itapatikana.. .. Bila ya kuwa Muislamu ni hasara na majuto siku hiyo.
Wewe sisi tuliofundwa iko hivi wakatoliki katika utiii tunatakiwa kutii nini? Tunalazima ya kutii mambo yote yaliyomema hatuna lazima ya kutii mambo yasiyomema yanayopingana kanisa katoliki .
Nyinyi wenzet mnatabik kwakitu hambacho kiko waz Sisi Waislam tuko kimya Uslam nistret hakuna mchezo kam nyinyi kwet hakun Baba mtakatif Sisi mtakatif ni Mungu Na Mtume Muhamad
Yaani huyu hana huelewa kabisa. Na mwandishi hajamuuliza kabisa maswali ya kuufunua ukweli. Hakuna mahali Baba Mtakatifu karuhusu kufungisha ndoa ya jinsia moja. Kilichozungumzwa ni baraka inavyotolewa kwa watu. Kama kuna sehemu Baba Mtakatifu kasema tufungishe ndoa za jinsia moja tafadhali nionesheni niione. Baraka inatolewa kwa wote kwa watakatifu na wadhambi.
Huyu anayehojiwa hata hajielewi na haelewi utaratibu wa kanisa katoliki...papa anapotoa tamko huwa limeshajadiliwa na makadinali wa dunia nzima..na makadinali hukusanya maoni toka kwa maaskofu...kuna kitu kinaitwa SINODI, unajua maana yake??sasa unaposema hapingwi una maana gani??? Halafu mbona unapitosha maelezo ya waraka wa papa?? Jua kwanza jambo k abla hujatolea maelezo.😢
Huyu mtu mbona amebadilika rangi alikuwa mweusi ghafla kawa zeru zeru lini jamani ? Kama vile kabadili sura au kavaa sura bandia ?? Nauliza tu maana nilimfahamu akiwa mweusi mwenye rangi nzuri tu ya maji ya kunde !!
Hakuna pa kushikwa pabaya, ukatoliki haujawahi na hautakuja kukubali ndoa za jinsia moja. Ukitaka kuwaona wanaojiita wanarohomtakatifu walivyo waongo na hadaa nyingi ni hapa . Mwone huyo anayejiita kiongozi wa makanisa ya kipetekoste, anavyopindisha ukweli kwa nia ovu. Hawa ndio wanaojiita watumishi wa mungu eti wameokoka , wanaongozwa na roho mtakatifu. Wachumia tumbo, ndio maana wanatengana kila uchao.
Kwani papa ni nani? Shida baadhi ya wakristo wana tabia ya kusahau maandiko, mfano, mathayo 23; 9-10. Hapo YESU alijua kuna mtu mwaribifu atakuja duniani na kujivika cheo cha MUNGU, neno papa, tafasili yake ni MUNGU, sasa mwanadamu kama huyo unawezaje kumwita mungu mtakatifu,, yaani papa mtakatifu. Hii ni hatari sana.
Tatizo ni mihemko tu, papa alikuwa anajibu swali la waandishi wa habari kuhsu ushoga, hayo yalikuwa maoni yake sio maagizo kwa kanisa, na hakuyazungumza kwenye Misa takatifu, wala hakutoa maagizo wala hakuandika waraka kwa kanisa, ni tafsiri za watu tu na chuki kwa kanisa katoliki lakini Mungu anajua yote na atasimama na kanisa
Mnakuza nambooo..ovyo! Hakuna ujinga huo kazi kutafuta kuzodoana tu ndipo watu mnapochelewa safar ya tumaini kuelekea mbinguni. Alafu mnamegukana tu,dhambi za ubinafsi na ubishano tu ovyoo!
kunahaja ya tec kujitokeza na kutoa tamko linalo ainisha msimamo na siyo kupakwa matope na mtu moja kumbuka kanisa lina taasisi ambazo jamii inahudumiwa hivyo kama kanisa likionekana kutaka kujionyesha balaka ambazo zinaleta mkanganyiko lazima litolewe tamko
ndugu hawa wanajadili habari kutoka bbc, hawajakwenda tec kuwauliza wamepata waraka wa namna hiyo kutoka kwa papa.. ofisi hazifanyi kazi kwa kutumia mitandao.. unapaswa kuwa na barua ya maelekezo ili uweze kuijibu. otherwise utatoa tamko kwa kila kitu cha mtandao
We muulizaji na anayejieleza. Munania ovu na kanisa katoliki, acheni uwongo na ushetani. Kawaulize maaskofu wakatoliki sio wengine kama hao. Angalia unayemhoji ni mkweli? Mbona hajielewi. Kanisa katoliki na baba mtakatifu hawajakubali ndoa za jinsia moja. Waulize hao kuhusu uvibwetele , umakenzie na uzumaridi. Huoni anavyohadaa kwa kurudia rudia jambo ambalo si kweli. Na anayeshabikia uwongo si mpenzi wa mungu. Eti wakae kikao ili watoe tamko kwa lipi? Wakatoliki wanawapa baraka watu wote. Huyo kama kweli ni wa makanisa ya kipentekoste basi anatunajisia neno pentekosite watafute neno lingine kwani haitaki kweli ni mwongo na anahadaa ni rafiki wa yule mwovu.
Sisi wakatoliki hatuna tatizo na maelekezo ya Papa kwani tumeelewa alichokisema. Shida ya watu ni pale wanapochukua neno moja tu kati ya mengi aliyoyasema Papa. Je, Yesu hakula na wenye dhambi? Je, Yesu hakumtetea yule mama mzinzi? Baraka zinatolewa kwa mtu yeyote yule bila kujali ana dhambi au hana dhambi. Lakini pia tukumbuke kuwa, dhambi si ushoga tu, la hasha. Kuna watu wana madhambi makubwa ya ajabu, lakini wakiomba baraka wanabarikiwa. Ni kosa kubariki ushoga, lakini si kosa kumbariki Shoga.
Zamani wakiristo wakiwakebehi waislamu ,kwa kusema ulawiti na usagaji ni michezo ya kiislamu ,leo Allah kawaonesha kumbe wao wakiristo ndio michezo yao
Tuna subiri Tamko kwa viongozi Wa kikristo sio mtu mmoja mmoja Kama walivyo kaa na kutoa waraka Kipindi cha swala la bandari Mbona kimya kigugumizi nini?
Nime kuelewa sana katoliki tanzania wanaona wao ndio wana hki watanzania kwa manufaa yetu sote wamepinga bandari ila ushoga kimya jitokezeni mbele mtujuzi je papa ni shoga au la
Martin Luther King (Bada ya kuisoma Biblia kwa Mara ya kwanza na kwa umakini- Alijitenga na taratibu za Rc ,Hali kupendeza Uongozi wa RC wa kipindi hiko wakitumia mamlaka ya kofia ya kisiasa walimkamata pamoja na wafuasi wake wakateswa na alikufa kwa kuchomwa moto ikiwa ni hukumu mbaya iliyowahi kutokea duniani bada ya Mitume na Manabii.
La bandari waliandika bonge la barua na likasomwa karibia makanisa yote 😂😂😂 ila hili wapo kimya kama mazuzu,any way huenda Papa kashapata mume (Ni msimamo wa Papa sio wa kanisa ila ajabu RC wanaogopa kusema)
Sasa kuhusu ushoga waandike Nini wakati hakuna maagizo waliyopewa? Unadhani mapadre ni watu wa kurukia uzushi mitandaoni? Yaani mzue uongo nyie na BBC halafu msubiri tamko ili iweje? Hawana muda wa kupoteza
Daa Kauli ni moja tu Yes or No.biblia imeruhusu ushoga? Kama ni No maelekezo yote ni ya nini.sijui baraka,sijui vitu gani...y nini yote haya Papa alipaswa kusema NO ushoga kanisa katoliki.simple.unapotaka kuleta maelezo mengi unaonekana unataka kuingiza hilo,jambo kidogo kidogo,maana baada ya kubariki atakuja na lingine,
Nilichogundua ni kwamba mwandishi wa habari anazo taarifa kwa kina kuliko Askofu Ikongo. Kwa ufupi Askofu Ikongo alikuwa anajibu kulingana na maoni ya watu aliyosoma mtandaoni, lakini pengine hajawahi kuiona taarifa yenyewe walau kwa lugha ya kiingereza
Huyu Askofu haelewi.Inaonekana ana chuki yake binafsi.Kutoelewa maelezo ya Papa ni uvivu wa kufuatilia mambo.Inaonekana tamko la bandari linamtesa.Hawa ndiyo wanaovizia anguko la kanisa katoliki.
sasa wewe ikongo umeshaambiwa haupo waraka wala barua iliyopo mezani kwa maaskofu kutoka kwa papa ambayo unataka waitolee tamko. wakiulizwa wameitoa wapi taarifa hiyo waseme tumesikia kutoka bbc na mitandao?? akili yako ndogo sana aise ndo unawaongoza wapentekoste kwa kutumia mitandao?