Baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo wameishauri Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) kuzingatia uthaminishaji rafiki wa kodi kuendana na gharama ya mizigo katika mpango iliyouanzisha wa kuweka bei elekezi za bidhaa zinazopitia bandarini kama ilivyo kwenye magari yaliyotumika.
Wametoa angalizo hilo muda mchache baada ya TRA kuainisha orodha ya bidhaa nane ambazo zitawekewa bei elekezi ya kodi zinapoingia bandarini ikiwemo vitenge na mashati ambavyo ni miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na wafanyabiashara hao kwenye mkutano wao na serikali jijini Dodoma ili kuweka urahisi wa ulipaji kodi.
Mhariri: @official_jennifersumi
#azamnewsupdates
29 авг 2024