Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu... Vile vile Yesu alitupenda akatoa nafsi yake kwa ajili yetu nasi tunafaa kujitoa kwa ajili ya wengine. Tuwajali, tuwapende na kuwasaidia wote wenye mahitaji. Umebarikiwa kuwaliko wote mtumishi.
Kwa mapenzi yako Mungu, kupitia kwa mwanao Yesu kristo, naomba unipe moyo wa kupenda na kujali wenzangu kwa kila hali. Unipe hekima jinsi ya majibu toka kinywa changu kwa wenzangu. Niishi kwa uhalisia wa kutenda kwa wenzangu na kulisoma neno lako kwa wingi.