Timu ya watumishi kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya imeanza vema michezo yake (Mchezo wa kuvuta kamba) baada ya kuichalaza Halmashauri ya Singida kwa pointi 2 kwa 0 na baadaye kuichala Halmashauri ya Magu point 9 kwa sifuli. Kwa matokeo hayo timu ya Chunya tayari imejikusanyia alama sita
Ikumbukwe timu ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya inatetea ubingwa wa Taifa mwaka wa tatu sasa katika Mchezo wa kuvuta Kamba na kwa morali ya wachezaji Ushindi lazima urudi Chunya.
Michezo ya SHIMISEMITA inaendelea huko jijini Mwanza kwenye viwanja vya Chuo cha ualimu Butimba
Unachatakiwa kufanya endelea kutufuatilia kwenye mitandao yetu ya kijamii
26 окт 2024