Тёмный

Dizasta Vina - Hatia V 

Dizasta Vina
Подписаться 52 тыс.
Просмотров 112 тыс.
50% 1

Official Music record of Dizasta Vina performing Hatia V
Written and Performed by Dizasta Vina
Produced by Dizasta Vina
Mixed and Mastered by Smart Jr Wonder
Music by Dizasta Vina
Art designed by Dizasta Vina
Videographer Baraka Graphics
Audio
Boomplay - www.boomplay.com/songs/112498...
Mdundo - mdundo.com/song/2163532
Audiomack - audiomack.com/dizastavina/son...
Lyrics - genius.com/Dizasta-vina-hatia...
Other Musical contents
Audiomack - audiomack.com/dizastavina
RU-vid - / dizastavina
Deezer - www.deezer.com/artist/67967532
Apple music - artists.apple.com/a/profile
Mdundo - mdundo.com/a/2263
Genius - genius.com/DizastaVina
Boom play - www.boomplay.com/artists/3288... - artists.spotify.com/c/artist/...
Connect with Dizasta Vina on social medias
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
sw.wikipedia.org/wiki/Dizasta...
Business: Pan.authentik@yahoo.com
Website - bio.link/dizastavina

Видеоклипы

Опубликовано:

 

25 дек 2022

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 825   
@kilingechasimulizi2072
@kilingechasimulizi2072 Год назад
Hakuna, narudia tena hakuna kwa wasanii wote wa tz anayefikia kichwa..hakuna
@kilingechasimulizi2072
@kilingechasimulizi2072 Год назад
Nilikuwa namaanisha hakuna wa kufikia hiki kichwa
@kyataonline5262
@kyataonline5262 Год назад
hakuna ! kwa nini hapati promo akaskika !
@emanuelmasanja8312
@emanuelmasanja8312 Год назад
Hapati promo wapi nani wapi hajasikika huyu kwa hapa hongo hayupo kama yupo mtaje jina
@emanuelmasanja8312
@emanuelmasanja8312 Год назад
Kyata! unajua misingi ya hip hop ama ndo whuzu na bonge la nyau
@kyataonline5262
@kyataonline5262 Год назад
@@emanuelmasanja8312 hapana siijui buda
@dizastavina
@dizastavina Год назад
LYRICS Yeah Nilimfahamu baba alikuwa jasiri Aliondoa utando ulipodandia kuta Alitoa nyoka makatili alipambana na Majangiri walipovamia nyumba Aliweka paa juu vichwa Hatukuogopa baa la njaa tulishiba Niliona wengine nguo za kuvaa zimechanika Wakati kwetu nyuso ziling’aa migongo ilifunikwa Radi ilipiga wala sikujali Maana baba alikuwa Simba kwenye msitu mkali Wapo waliozijua sifa zake japo Mtaani halikuwika jina lake Halikuandikwa bali Waliona poa ilikuwa jukumu lake Mwanaume jasho kutoa ndio hukumu yake Ajali ya kisu iliondoa ngozi Sikumwona akitoa machozi Nilimwona kama Role model Alikuwa shupavu hakuwa na roho ndogo Mara chache alianguka ali-score zero Alipambana upya kama war Hero mdogo mdogo. Maisha yake yalikuwa ni adventure Alikuwa ni Handyman Carpenter Painter Alinijuza aliyoshuhudia kwa macho Maana Aliisafiri dunia enzi zake kama Vasco Alikuwa so gentle Alimpenda mama kupita maelezo Watu walijadili nini maana ya upendo Waliunda dhana mi niliiona maana kwa vitendo Huh Ugonjwa uliingia mama aliugua maradhi Homa ilivamia ghafla kupumua kazi Baba ali-suffer Hospitali kadha wa kadha Changamoto afya kupigania zikafungua jamvi huh Hali ilileta mtiti Hakuipata nafuu ugonjwa ulimweka kingi Baba aliwapa Waganga wakuu pesa nyingi Mixer kupelekwa majuu zinakoendeshwa ligi Mama alilala hospitali miezi kumi na nane Nyumbani miezi ilikuwa ni kama karne Tulimzoea mama baba hakupagawa Alisimama imara japo mambo hayakuwa sawa kamwe Maisha yalibadilika tukabadilika pia Familia ilipata shida ila baba aliisimamia Ukubwa ulimshika majukumu yalishika njia Yalimkaba shingo ila sikuwahi kusikia analia Bahari ikichafuka inampima nahodha wa meli Kama ataogopa kufa au ataongoza Kweli Lakini si mawimbi samaki waliododosha meli Bali ni rafiki wa karibu wa mama anaitwa Mary Mary alimjali baba alimzidi Rose Alimzidi Rahma alimzidi Shosi Alimletea baba kadi aliniletea chopstick Alifua nguo aliosha vyombo na alipika msosi Aliingia mpaka chumbani kwa mdingi Na udhaifu ukaanza yumbisha misingi Mary alimshawishi baba baba akaingia kingi, Kwa muda akamsahau mama akapitiwa akamsaliti ah Hamu ya tendo ikawazidi maarifa Kijakazi akazibeba taarifa Miezi kadhaa baada ya mama kupona Akasimulia yote aliyoyaona kama picha Mama akatokwa na machozi Baba akasota kwa magoti Mbele yangu mi mwanae mbele ya wazee Wakunga wa ndoa wenye busara waliobeba koki Huh Mama akapata mashoga wakali Walitoka jangwa la Sahara na Kalahari Wenye elimu za kutosha na ajenda kali Wakamwambia talaka ukiomba utazipata mali Mama akiwa na chembechembe za hasira Akashawishiwa na wasomi wenye hira kwa mbali wamezongwa na tamaa za ngawira Akasahau kumsamehe kama ilivyosemwa mila Mama akafungua jarada la talaka Akaandaliwa Majeshi waliojipanga kwa karata Baba aligoma kutoa talaka akiomba wamalizie nyumbani sio mahakamani na mama hakutaka Mji ulifahamu kesi iling’ara Yalipambwa magazeti mengi kwa nakala Wanaume washenzi waliongea wapambe Vijiwe vya uswazi waligawana pande ka masihara Mzee hakukataa mwisho akakili kosa Talaka ikaidhinishwa ndoa ikadondoka Baba akapata uchungu likamshukia rungu Kisha mama akaonyeshwa fungu akachota Afya ya mama ya uchumi na mwili vikanawiri Akawa Malkia mji ukatabiri Baba akawa kama kifaranga kwenye mvua Bado alimpenda mama na mama hakujua Mama aliitwa Superwoman ama soja Aliushinda usaliti aliushinda ugonjwa Baba alimkosa mama kwa starehe ya usiku mmoja Alimpenda mama hivyo kumpoteza maumivu tosha Washiriki wa biashara walimweka kapuni Akafukuzwa kazi asiharibu sura ya kampuni Vikundi vya kina mama walisherekea kombe Dingi aliipoteza kazi akaisogelea pombe Hakuwa sawa kichwani aliishiwa Energy Hakukuwa na counseling hakukuwa na Remedy Zaidi Makala zilizoandikwa na Mafeminist Pesa zilimwisha mtaani alifuga Enemies Magazeti hayakuandika alivyokuwa hero Yaliandika matusi yaliyomzidi kilo Aliitwa Malaya shenzi katili Mwanahizaya mwenye cheti cha ujangili Na yakapiga millions Hakukuwa na vyama vya wanaume kumtetea baba wakasema ana pepo la uzinzi Ustawi wa maisha yetu ulipotea ghafla Wanasheria wakala na pesa za ushindi Aliumia peke yake Dunia ilimweka peku Dhambi ilimwacha uchi hadharani Alifanya mema zaidi ya kumi hayakutosha awe Yesu Ila baya moja aliitwa Shetani Alizubaa Alizubaa na akashikwa na madoa Alikuwa shujaa ila alishindwa kujiokoa Mwamba wa nyenzo ya katikati ulipoondoka Ilimaanisha ni muda wa Safina kudondoka huh Hazikusikika sifa zake njema Machozi hayakusafisha jina lake tena Haiba alizokuwa nazo hazikuvutia kamwe msongo nao wa mawazo ukamvamia Mfalme Aliandika barua ya hadithi yake Akisema kilichomtesa sio dhiki yake Bali ni uzito wa alichokifanya Alijiua kando ya bahari uliokotwa mwili wake
@umodernize4142
@umodernize4142 Год назад
You
@alphanlukombe3774
@alphanlukombe3774 Год назад
Hii kali sana hili ni fumbo tuliolielewa watu wachache sana nakubali sana dizasta vina katika uandishi wako mtu akisikiliza juu juu anaweza akaona kawaida lakini hii Ngoma umeimba mambo makubwa sana kwa sisi waelewa dizasta vina on top
@reganmmasi1246
@reganmmasi1246 Год назад
Sasa mkuu mbona pale spotify kama umetutenga hiv...😕😕
@jebajr
@jebajr Год назад
Always upo tofauti sana na hawa wasanii wetu, wewe ni sanaa.
@dizastavina
@dizastavina Год назад
@@reganmmasi1246 ipo njiani
@jolamboi8842
@jolamboi8842 Год назад
Dah dizasta ndio my favorite rapper ebu tupia like kama una mkubali mwamba 🔭
@nillyjos1203
@nillyjos1203 Год назад
Daah kaka Tanzania nsima wew Ndo msani Bora Tanzania nzima
@mtunda_thegreat_thinker
@mtunda_thegreat_thinker Год назад
Daaaah broh wewe ninomaaaa sanaaa 👊👊🔥🔥🙏🙏 tunao mkubali dzstvn tujuane kwa likeee hapaaa
@timothykaiza327
@timothykaiza327 Год назад
Iko Auto playing saa mbili sasa, ni ngoma yangu ya leo kutwa mzee. Tunaozidi irudia HATIA V tukutane hapa. Nitumie mimi kama kitufe cha kukubali ujumbe huu.
@kaissalum7364
@kaissalum7364 Год назад
Duh bro sina mengi ebu weka namba Nikutumie chochote kitu nakukubali sana
@stonestz8815
@stonestz8815 Год назад
Dizasta dizasta dizasta ndo toleo la mwisho la viumbe aina ykooo
@revocatusnzungu6580
@revocatusnzungu6580 Год назад
huwa natamani kila mwezi jamaa atoe ngoma dah ... kuna watu tuna arosto na ngoma zako broo dizasta
@penuelobeid9857
@penuelobeid9857 Год назад
Wimbo wa dakika 8, hauongelei siasa wala mapenzi... Story fulani iliyotilia kuhusu familia. Dizasta Vina is the Legend🔥
@renatusmsakula4746
@renatusmsakula4746 Год назад
Anaetaka kujipima na wewe hatokua SAFE yaani no body is safe!!!
@Mr.Kibabu
@Mr.Kibabu Год назад
Dizasta hajawahi niangusha, Kichwa kweli kweli, Huwa na Like kwanza ndio naanza kusikiliza, Msanii wangu Bora wa HIP HOP
@ablemuxic7334
@ablemuxic7334 Год назад
Kwa mwaka huu hii ndo nyimbo yangu bora ahsante Sana D 🔥🔥
@stevenjohn7816
@stevenjohn7816 Год назад
Hii ni film iliyokamilika kabisa bongo muvie karibuni
@millardmbaraka6114
@millardmbaraka6114 Год назад
Alafu anatokea muhuni mmoja anamlinganisha D vina na makinda dah! Umejua kutufungia mwaka na tafakuri murua kabisa
@joshmangi
@joshmangi Год назад
Hizi juhudi zinahitaji malipo, weka lipa namba watu wachangie hizi juhudi.
@valencepaul4604
@valencepaul4604 Год назад
Uliletwa kwa ajili ya HIP HOP wengi wamefichwa wewe ni nani ila ni zaid ya rapper zaidi ya mwalimuu wa jamii,,,,napo play ngoma zako hadi wazee wanauliza huyu ni nani😀💥💥UNAJUA SANA MIMI NI MFUASI
@johannesjoseph7496
@johannesjoseph7496 Год назад
Hakika unadhihirisha kwamba unaishi kwenye dimensions ambazo miungu ndo inasettle..... Hatia 1-5 zote mwisho wa siku lazima ujiulize nani alikosea zaidi..kila muhusika anakua na excuse ya kutenda makosa ijapokua uwezo wa kuyaipuka unakuepo japo mdogo kulingana na mazingira, I salute you our best storyteller the verteller
@reeckstar931
@reeckstar931 Год назад
All way from Switzerland 🇨🇭🇨🇭🇨🇭 nnasubili chakula Cha ubongo
@reeckstar931
@reeckstar931 Год назад
😭😭 kwanini wa bongo hawaamki kumpa sikio dizasta
@shehakudura3243
@shehakudura3243 Год назад
Aisee kwenye taswira ya kifamilia,,,, W,ume tujipe Poole,,, coz hakuna mafanikio ya watoto na family kiujumla bila Baba kusmama vyema,,, Ila aisee shiida ya UMUHIMU WETU kutoonekanwa na kuthaminiwa na KUTENGWA kwa KOSA Moja aisee,,, INAUMAA SANA....
@petercharles8572
@petercharles8572 Год назад
Kwenye harakati za kumpandisha mwanamke kuwa sawa na mwanaume zimekuwa harakati za kumkandamiza sana mwanaume na sio tena kumuweka mwanamke awe sawa na mwanaume... Dizasta ametuonyesha jinsi mama alistawi kutokana na dunia nzima kuwa upande wake na baba hakusikilizwa. This man deserve 01, Ni jambo la kujivunia kuwa wakati mmoja na dizasta vina... Bahati mbaya kwa wote waliotamani kumsikiliza msanii kama huyu ila hawakufanikiwa kwasababu waliku past na records hizi mustakabari mzuri kwa kizazi kijacho. We love you Dizasta Vina
@dizastavina
@dizastavina Год назад
Feeling is mutual, cheers
@richardmloha1762
@richardmloha1762 Год назад
Jamaa n anaumiza ndongaa wazee kwanin lakin ngoma Kama hizi watu wake wanashindwa kuwa na maslahi yanayoendana na hustles zaoo daaah 😓 em sisi mashabiki tuanze na hii ngoma iangalie ata Mara 5 utatisha sanna let's go
@Makavelithedon2086
@Makavelithedon2086 Год назад
*Dizasta Vina ni moja kati ya best lyrical rapper kuwaikutokea Tanzania*
@shariffahmad8705
@shariffahmad8705 Год назад
Kama messi alipata alichostahili kwa miaka yote hiyo amini ndugu yangu utapata unachostahili one day keep it on unajua mpaka unajua tena akili mingi mtu wangu
@alimkumba9459
@alimkumba9459 Год назад
mtu yeyote anamsikiliza dizastar naamini hatoweza kuupoteza mziki wa huyu mwamba kwenye kuta za sikio zake nahisi huyu sio mtu wa sayari hii
@selemaniselemani591
@selemaniselemani591 Год назад
Haichoshi kusikiliza Leo hii ni mara ya 16 bado Radha ni ile ile Kama ile Ngoma ya tattoo ya asili bro wewe ni nyoko naomba nikusifie kabla hijafa wewe ni nyokooooooo🔥🔥🔥🔥
@gwaphototv2046
@gwaphototv2046 Год назад
Hii ni zaid ya Wimbo bora wa Mwaka kaka, Funzo,Vina na 🔥🥂
@morganmwaikusa8194
@morganmwaikusa8194 Год назад
Genius.... Huyu Edgar anajua mpk anakela yan....
@francismasanja5550
@francismasanja5550 Год назад
This talented man should be crowned. What a good music, what a strong message. This is what a literature is and means.
@amalillahasante6693
@amalillahasante6693 Год назад
Trust
@johnizoboy
@johnizoboy Год назад
Very true🔥🔥🔥
@aplus3805
@aplus3805 Год назад
yapyap
@ShabaniAbdi-q1w
@ShabaniAbdi-q1w 23 часа назад
Nomaaa sanaa
@hurumamwankuga6663
@hurumamwankuga6663 Год назад
Style yako Ime inspire rappers wengi but hiyo hiyo style Iko tofauti na wao bcz unavyotema na wanavyotema there are so different 👐👐
@erastompongo8400
@erastompongo8400 Год назад
Duuuh we jama ni mnoma sana wangapi wanailudia rudia
@odiloodilo
@odiloodilo Год назад
Me nishabiki yako sik zote, kaka upo vizuri sana 👍💯💯💯💯🙌
@jacksonkitosi6504
@jacksonkitosi6504 Год назад
Kwann nilichelewa kumjua huyu mwambaa brother be blessed 🙏 🔥 🔥 Unajua sanaaa
@mtaaruma
@mtaaruma Год назад
Kweli mazuri kumi hayawezi kufanya uitwe Yesu but baya moja utaitwa shetan The game is in yourself hands prf tungo
@braytonedaniely7977
@braytonedaniely7977 Год назад
Tym yako ndo hii mwanetu utaeleweka tu siku moja✌
@rogathpanga
@rogathpanga Год назад
Yaah Nilimfahamu baba alikuwa jasiri
@filbetdaud4597
@filbetdaud4597 Год назад
mamaeh aisee iki n kichwa na nusu aiseee Mzee D unaandika sana unaandika sanaaa kaka unaandikaaaa nasemaaa unajuaaa sanaaa D ish sana mflame D
@mbarakamngayunga9558
@mbarakamngayunga9558 Год назад
Daaaah,aisee sikutegemea kama ningekutana na idea kali kama hii...wewe brother dizasta ubarikiwe sana...Nyimbo zako zinanifunza sana❤
@octavian54
@octavian54 Год назад
Unafelii wapi huyo ndio Mwenye mziki wa hip hop
@amalillahasante6693
@amalillahasante6693 Год назад
Kweli mwanangu.
@babamasakalanga5687
@babamasakalanga5687 Год назад
Daaah hii ngoma imenitoa chozi nimekumbumbuka mbal sana😭😭😭😭😭
@idrissachisigwa5360
@idrissachisigwa5360 Год назад
Noma sana
@shehakudura3243
@shehakudura3243 Год назад
@@babamasakalanga5687 for real Yani inaniumiza sana hii ngoma aisee,,,, W,ume thamani yetu mbinguni ila tunavuja Jasho hatari lakin mwishoe tunaambulia kisukari na presha
@yusufuselemani6339
@yusufuselemani6339 Год назад
Good work kutoka kwa narrator bora wa mda wote, Sema D humu na muona hayati kabisa kazungumziwa 😀😀
@danielmbilinyi4025
@danielmbilinyi4025 Год назад
Huaga najaribu kuandika mistari ila nikimsikiliza Dizasta vina najiona siandiki kabisaaa
@sayedkhamis5204
@sayedkhamis5204 Год назад
Bro una akili Kubwa wewe sio msanii wewe sio Mwana Muziki wewe Ni Legendary wa Maandishi, sauti na Midundo The Story Teller Never Seen Before Keep Pushing Vinna
@lukona5821
@lukona5821 Год назад
Dah sijui kwanini nimeusikiza...Nimeishi katika hyo mistari kama natazama movie...Umeniacha na Majonzi mjomba but...Yeah Nilimfahamu baba alikua jasiri....Wapo waliozijua sifa zake....Mtaani halikuanzikwa jina lake.....Alifanya mema zaidi ya kumi hayakutosha awe Yesu...Ila baya moja aliitwa Shetani Alizubaa...WOW
@erickpaschaljr8667
@erickpaschaljr8667 Год назад
Ninamshukuru Mungu kwa zawadi ya mziki mzuri wa Dizasta vina yawezekana sisi ni watu wenye bahati sana ila bado hatujatambua thamani ya utunzi usio wa kawaida.
@ibrahimnjohole1684
@ibrahimnjohole1684 Год назад
Daaah....huyu msenge anachora nyinyi.Ishi sana mzee baba.Huu ni zaidi ya mziki.
@idmpros
@idmpros Год назад
nomaaaa sasa @dizastavina wewe upo mbeleeee sanaaaaa ya Muda Trust me watu ni kama hawakuoni BUT I BELEAVE IN GOD TIME WATU WATAKUZINGATIA KWA KISHINDO
@isdoryemily5029
@isdoryemily5029 8 месяцев назад
Uyu mwamba amejua kunibadirisha sinaga mshauri nyimbo zake nikisikia najifunza na mtaani naitwa Hip Hop culture
@ahmedramadhani1264
@ahmedramadhani1264 Год назад
Binafsi nimeisikiliza zaidi ya mara tano kwenye simu na bado naendelea kuisikiliza. Noma sana hii kitu.
@ahmedsdk6736
@ahmedsdk6736 Год назад
Ya Moto sanaa Hiii... 🔥🔥🔥
@dizastavinafanaccount
@dizastavinafanaccount Год назад
Sanaa yenye usanii. Mwendazake Mr Magufuli. Akitenda kosa lakini upendo na uzalendo wake kwa hili taifa ulikuwa juu ya maelezo. Dizasta amesymbolise kupenda na kujali ni kama kujiua mwenyewe. Kalamu ya Dizasta si ya kawaida
@CertifiedStoic
@CertifiedStoic Год назад
I remember 27th December last year i got myself a copy of ‘The Verteller’. I promised myself to keep on buying Dizasta Vina’s art at any reasonable cost. All hail to the King of Underground 🙌💪
@mtasma1994
@mtasma1994 Год назад
Mimi huwa simfananishi Dizasta na Rapper yeyote
@mkanganails5839
@mkanganails5839 Год назад
Daaa aisee unabalaa zito wewe una hatareeee mwamba
@g_eazmusic1329
@g_eazmusic1329 Год назад
Kosa moja mtu anasaau wema wote
@raymondedson2488
@raymondedson2488 Год назад
Sehem moja ya kuufungua ubongo WA vijana ni kupata hadithi na zimulizi kama hizi Hakika we ni mwalimu WA fasihi na si mwalim Bali mwandishi bora WA muda wote katika game much respect brother
@jumazinga941
@jumazinga941 Год назад
Ama kweli baba atabaki kuwa hero
@topaztz7601
@topaztz7601 Год назад
Mwanangu wa Faida, Dizasta Vina 🔥🔥🔥🔥📍📍
@fabycreation1962
@fabycreation1962 Год назад
DIZASTA VINA 🙌🏿 usiku mmoja umebadili fomat yoot y maisha duh 😔
@mansourabdul3902
@mansourabdul3902 Год назад
Keep it up aisee unaandika leo ndio mara yangu ya kwanza kuusikiliza na kukujua ila sasa nihesabu kama shabiki yako sasa
@macberryofficial
@macberryofficial Год назад
Ooh i have been just listening to your song SHAHIDI and NDOA, and i just see this one😊😊😊 man Dizasta i love your songs fasho! Huyu ni Fan wako kutoka 🇧🇮Burundi🇧🇮 hujawai kuniangusha Dizasta Vina😊💪💪💪
@lunyatheprodigy
@lunyatheprodigy Год назад
Nashukuru Mungu nipo zama hizi kushuhudia hiki kipaji...
@raphaelmwangosi9295
@raphaelmwangosi9295 Год назад
Kak daaaaaaaa cjui tusemeje mwanang ila bc wameweka tasnia chino ila tunakuexhmu 💪💪💪🥰😍🥰🥰🔥🔥🔥💥💥💥
@mr.theory5871
@mr.theory5871 Год назад
Oyaaaaa mwamba anaandika hadi anaandika tena,cha ajabu tuzo kwa wanaosifia ngono!
@FourTeen_Kiid
@FourTeen_Kiid Год назад
argentina wana messi bongo tuna dizasta vina the black maradona 👏🏾🙌🏾🔥
@gervasscofield
@gervasscofield Год назад
TUNGO TUKUFU 🙌🔥 BEST RAPPER OF ALL TIME (Greatest Of All Time) G.O.A.T @dizasta 🧡
@moureennassoro1048
@moureennassoro1048 Год назад
Jamii imeshiba sana ujinga dats why you are not fumes. Dizasta vina ni mmoja tu Dunia nzima. Huwa anazaliwa mmoja tu toleo la aina yako. Dizasta vina, unasikilizwa tu na watu wenye akili timamu. Busara ipo moyoni, hekima ni busara inayozungumzwa. Dizasta vina, naandika jina lako kwa heshma kubwa zaidi ya ninavyolitamka. Dizasta vina, begani mwangu jina lako nitalichola tatuu , najivunia msanii wangu na sio 2pac Shakur Dizasta vina. Usisahau kuwa wakati unasifiwa, bado hauko kwenye njia yako mwenyewe, bali upo kwenye njia ya kupendeza kwa wengine. Hapo namaana kuwa bado nataraji kushuhudia kazi zako nyingi na za hatari zaidi ya tunavyokujua sis Media wanaogopa nyimbo zako
@jibrilsheikh9949
@jibrilsheikh9949 Год назад
Huyo jamaa Ni Noma... This is pure talent ❤️❤️❤️. Tunapenda kazi zako Safi Sana kutoka Kenya
@oscarsospeter3998
@oscarsospeter3998 Год назад
Hayawe hayawe Yamekua Wanapo ishia kufikilia Ndipo Sisi Tunapo Anzia
@peterbahati924
@peterbahati924 Год назад
This is the real meaning of Hip-Hop. He is the real meaning of Rapper, doing things never been done before🔥🔥
@charleskitoki4648
@charleskitoki4648 Год назад
Brother hujawai niangusha hakika hicho kichwa ni hadhina ya Taifa 🔥🔥
@ausiissa7155
@ausiissa7155 Год назад
Kuna mda uwa nikisikiliza nyimbo zako nikisema unajua naona Haitoshi inabidi tu niwambie wasio kujua kwamba unajua ili wao pia wakatoe ushuhuda ✨✨Mungu akuweke sana kaka✨✨
@StimaOfficial
@StimaOfficial Год назад
Sijawah kuchoka kuzipakua na kuskilz hizi punch mzee wa Panorama Professor Tungo💪💪💪
@joycelugenzi1889
@joycelugenzi1889 Год назад
Kaka mm cjui ata niseme vp .but nakupenda xana i wish nipate mda wa kukuona hata 2ongee nahisi ningejifunza mengi kuhusu hii dunia .nimeipenda xana nyimbo .😍😍😍
@dedeayew9650
@dedeayew9650 Год назад
Ambae hatapenda hizi lyrical aisee huyo hajui music
@ibrahimukasimu3386
@ibrahimukasimu3386 Год назад
Kaka shikamoo we unajua mpaka nawaza kuwa haujatoka latina hii planet dah uno amor amigo god bless u on ur evry step of ur lyfe
@mwangumwangu1599
@mwangumwangu1599 Год назад
I appreciate you brother.... We jamaa ni nomaaaaa udumu mileleee
@SirMasalu
@SirMasalu Год назад
Kila ukitoa ngoma, unatupa fundisho but hii ni zaidi ya darasa 🙌🙌🙌
@macpharaonofficial269
@macpharaonofficial269 Год назад
Hiki chombo Cha mistari vina hua nakikubali siku zote🔥🔥🔥 keep shining Brother ✌️✌️✌️
@abdulkara2327
@abdulkara2327 Год назад
Kutoka Zanzibar kama unamkubali dizasta gonga like mwanangu kumaanisha huyu jamaa ni mwamba
@delymoebright9326
@delymoebright9326 Год назад
Tulio elewa kilicho imbwa tujuane dah🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
@johnngowi8334
@johnngowi8334 Год назад
Noooma sana aisee , wew ni mkali saaana hapa bongo unandika sanaaaa⭐⭐⭐⭐💥
@revocatusnzungu6580
@revocatusnzungu6580 Год назад
Ningekua mwalimu wa kiswahili nyimbo za Dizasta zinastahili kufundishia kabisaaa ......na kama nikija kuwa waziri wa elimu nyimbo za Dizasta zitatumika shule za sekondari na elimu ya juu kufundishia
@kilingechasimulizi2072
@kilingechasimulizi2072 9 месяцев назад
Kama nyimbo ya shahidi
@laxmajor
@laxmajor Год назад
Unyama mwingi kizazi Sana 🚀🚀🚀🚀
@mkolekulwa3090
@mkolekulwa3090 Год назад
Kama upo kwenye ndoa hili ni darasa kwenu. Dizasta genius
@mtupakiemba5016
@mtupakiemba5016 Год назад
Dizasta genius, jamaa ubongo wake ni watofauti sana na wasanii wengine kila cku anatupa mafunzo mapyaa ktk jamii ilele ya cku zote.......this man🔥🔥🔥
@binamour6247
@binamour6247 Год назад
Daah we jamaaa madini ni mengi kichwani. 🔥💥💥💥🔥
@worldhappiness1181
@worldhappiness1181 Год назад
Mwandishi Bora wa Muda wote Tanzania
@stevemwachi254
@stevemwachi254 Год назад
Nikiona umedondosha dongo,najua nimda wakusoma maisha...Bro utunzi wako hauna mfano..Kichwa kimoja akili za watu million 1..super natural talent..
@igpk2275
@igpk2275 Год назад
Dizasta wew ni 💥💥
@yojoruta3379
@yojoruta3379 Год назад
Genius artist of Africa continent ebu fanya collabo na Kendrick lamar na J cole ao ndo level zako mkipga ngoma moja itakuwa super hit all the time in the world
@revocatusmgusi4479
@revocatusmgusi4479 Год назад
Atawafunika wote
@jjokochamwakyusa3626
@jjokochamwakyusa3626 Год назад
Daaaaah baya moja linafukia mema zaidii ya 1000 hii htr
@ommyrama4814
@ommyrama4814 Год назад
Wimbo mkubwa sana aiseee MUNGU akupe stahiki yako ya eshima katika muziki huu
@amaningasa9536
@amaningasa9536 Год назад
The black maradon.. Ujawai niangusha bro this is the story teller
@immanuelmwaipopo1144
@immanuelmwaipopo1144 Год назад
Mbeya we are proud of you bro
@emanuellawrence7462
@emanuellawrence7462 Год назад
T.I.A legend
@kelvinchuhila3780
@kelvinchuhila3780 Год назад
Best story teller ever in east Africa
@awardbillboard
@awardbillboard Год назад
Mema 10 aliyofanya hayakutosha kuitwa Yesu. LAKINI kwa baya moja anaitwa Shetani.... Jamii ipo Ivo 🥺
@johnizoboy
@johnizoboy Год назад
Huu uandishi ni zaidi ya Hisabati🔥🔥🔥🔥🔥Huu ni zaidi ya Wimbo🔥🔥🔥🔥This Guy deserve a Crown🔥🔥🔥🔥Anafanya Rap ionekane kitu chepesi sana kuisikiliza, Story Complex yenye Flow na Rhythm tanu sana🔥🔥🔥🔥ni zaidii ya Fundisho🔥🔥🔥Kuwaunganisha Fanani na Hadhira kwa Dakika 8 na kuelezea tukio ambalo limetokea zaidi ya 10+ is next level🔥🔥🔥🔥🔥Absolutely Perfect🔥🔥
@choineymar9765
@choineymar9765 Год назад
Phenomenon lyricist
@jebajr
@jebajr Год назад
Kiufupi tuwe tunafanya malipo kusikiliza hizi tenzi
@johnizoboy
@johnizoboy Год назад
@@choineymar9765 Absolutely
@AmisiHassaniTygo
@AmisiHassaniTygo Год назад
Daahh, kuna watu wana Chana nyie
@josephmsingi6226
@josephmsingi6226 Год назад
Brother sina neno kwako🙌🙌
Далее
Dizasta Vina - Hatia VI
7:02
Просмотров 52 тыс.
Dizasta Vina - Shahidi
6:38
Просмотров 181 тыс.
Beautiful gymnastics 😍☺️
00:15
Просмотров 7 млн
Dizasta Vina - Wimbo usio bora (Official Music Video)
5:13
Dizasta Vina - Muscular Feminist
9:05
Просмотров 99 тыс.
Dizasta Vina - Hatia IV
7:37
Просмотров 154 тыс.
Dizasta Vina - Nobody is safe 2
5:18
Просмотров 72 тыс.
Shaulin Seneta -Mtaa Na Shule
4:37
Просмотров 9 тыс.
Tribulation
11:27
Просмотров 21 тыс.
Slow Dance (feat. Sofia Carson)
3:09
Просмотров 878 тыс.
АМ АМ
1:31
Просмотров 262 тыс.
지민 (Jimin) 'Who' Official MV
3:28
Просмотров 12 млн
Mirjalol Nematov - I love you (Videoklip)
3:56
Просмотров 2,7 млн
KIZARU - OBUZA
2:25
Просмотров 218 тыс.