Gavana wa Kaunti ya Samburu Lati Lelelit amelaumu usimamizi wa kampuni ya usambazaji umeme nchini ya KPLC kwa Mikasa ya moto iliyozuka mjini Maralal wiki iliyopita. Gavana Lelelit anataka usimamizi wa kampuni hiyo kuwajibikia Mikasa hiyo ya moto iliyoteketeza bweni la shule ya upili ya vijana ya Krisia pamoja na biashara mjini Maralal na kuwaacha wafanyibiashara kukadiria hasara ya maelfu ya pesa.
16 сен 2024