Watu watatu wamekutwa wamefariki dunia kwa kuchomwa moto na watu wasiojulikana eneo la msitu wa Hifadhi ya Korogwe Fuel, uliopo Kijiji cha Sindeni wilayani Handeni mkoani Tanga.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 24, 2024 kuhusu tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema tukio hilo limetokea jana Septemba 23, saa tatu usiku.
Amesema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuwatafuta wahusika.
Kamanda amesema walipokea taarifa ndani ya msitu huo kuna gari ndogo inaungua moto na pembeni yake kuna watu wawili wanaungua.
Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi
24 сен 2024