[20:59, 17/09/2024] +255 713 404 214: Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limetoa taarifa ya awali kuhusu mauaji ya watu watatu, ambapo imebainika kuwa walipoteza maisha katika nyumba moja baada ya kuchomwa moto, huku mmoja wao akipigwa na kitu kizito kichwani.
Akizungumza leo, Septemba 17, 2024, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, SACP Anania Amo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa liligundulika Septemba 16, 2024, saa tisa mchana, katika Mtaa wa Segu Bwawani, Kata ya Nala jijini Dodoma.
Kamanda Amo aliongeza kuwa uchunguzi wa chanzo cha tukio hilo bado unaendelea, huku hatua za kina zikichukuliwa ili kubaini wahusika wa mauaji hayo.
Tukio hili limezua hofu miongoni mwa wakazi wa eneo hilo, huku Jeshi la Polisi likiendelea na msako kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
[21:19, 17/09/2024] +255 713 404 214:
18 сен 2024