Ahsante mama. Mbali ya hizo kazi zako nakunasihi ifanye Quran rafiki yako mkubwa. Jaribu kuisoma na ufahamu tafsiri yake na ikuwezekana fanya bidii ya kuhifadhi japo kidogo. Ukweli itakutibu stess sana na kukusaidia kwa mengi. Tafsiri ya Quran kwa Kiswahili inapatikana mtandaoni ya Sheikh Ali Muhsin. Maisha mema
Samahani sana lkn inabidi tuseme ukweli ili watu waweze kujikwamua mana wengi husikitika stress/upweke na mwisho wake baadhi Yao huishia magomjwa ya akili, Allah atuhifadhi sote, amiin
Alhamdulillah 'alaa kuli hali. Pole dada kwa huo upweke ni ngumu sana maisha ya ng'ambo mswahili ni kiumbe ameumbwa kuishi na jamii kwa furaha na amani.
Wa Aleykum salam sister Jamila na mimi na ndugu zangu tunakupenda fi Allah daima twakutaja kwa kheri unatuchekesha Jazashi'Allah kil'kher Allah akufanyieni wepesi na faraja katika kila gumu Liwe jepesi🤲 Kwa kweli sisi binadam tupo kwenye mitihani popote utapoishi ulimwenguni ikiwa kwenu au ugenini - Lamuhimu tuwe na Subra - Allah anatupa mitihani anatupima Imani zetu either tushukuru or tukufuru - tunamuomba Allah atuvushe salama kwenye mitihani anayotupa ya duniani na ya akhera na atujaalie khatima njema tuingie peponi In'Sha'Allah. ILa tujitahidi na silaha tatu za muhimu iLi tupambane na maisha - yakwanza ni (Iman kwa Mungu), Tuamini kuwa m'mungu ni mmoja hakuna mwingine na yeye ni muweza wa kila kitu Kwahiyo daima tumtegemee - na mwenye kumtegemea m'mungu anamjaalia milango ya faraja La muhim tusichoke kumuomba na kumuabudu. - Silaha ya pili Subra, tumuombe Allah atupe Subra fa Inna Allah masabrin m'mungu yupo na wenye kusubiri - Na silaha ya tatu Shukur kwa Allah, Daima tumshukuru Allah kwa kila kitu kwa furaha na karaha, tumshukuru kwa kila neema yoyote alotupa japo ndogo yaani tukinai - neema ya kwanza na muhim sana neema ya Uislam na kitabu chake katushushia Qurani wache tuijaalie iwe rafiki yetu inatupa Subra, raha ya nafsi, inatufungua akili, inatupa maarifa ukiifaham, na inatufundisha tusoyajuwa ya kumridhisha m'mungu. Tumshukuru Allah akitupa Afya, kwani wengi hawana upweke wame zungukwa na ndugu na majirani Lakini hawana Afya, hawawezi hata kutoka nje ya Nyumba na kuwatembelea watu. kila tukiamka asubuhi tuseme Alhamdulilah bado unaishi na una afya njema. Sister Jamila mashallah M'mungu kakuumba mzuri, bashusha, mcheshi na una imani, kakuruzuku mume na watoto you have nice family Alla ibarik mashallah mupo pamoja, mupo happy Alhamdulilah Allah akulindeni na kila mabaya In'Shaa'Allah wengi hawajaolewa au wameolewa Lakini hawana watoto - nakama usemavyo these days kuna mitandao ina turahisishia mengi Alhamdulilah tunaonana kwa sauti na picha tunashea online ikiwa sherehe or masomo upo nyumbani kwako Lakini unahudhuria live, bila ya kuhitajia kutoka au kuhitajia gari, wala safari yaani wajib tuseme Alhamdulilah rabil'alamin 🤲 kulinganisha na zamani mtu akisafiri hawawasiliani ILa kwa baruwa uifate post kama unamiliki postbox Otherwise inapita miaka mpaka iLi muonane tena mkijaaliwa uhai. Subhanallah kila jambo lina kheri yake Bora uko kivulini unakula na kulala pazuri wenzetu wapo vitani wakiishi Leo hawadhamini kesho - Let be positive huo upweke Labda Allah anakuepusheni na mengi mabaya na hasa huko hakufanani na mazingara yetu kama usemavyo - tusichukie kitu Labda kina kheri na sisi - tuchukulie kuwa upweke ulikuwa kama sababu na chanzo cha kuzinduka na kuchukua uamuzi upate kujishughulisha kwenye manufaa na In'sha'Allah yawe manufaa ya duniani na akhera - Mathalan faragha imekupa fikra ya kujilewaza na kulewaza wenzako kwa njia ya mtandao unatuchekesha tunafurahi unapata thawabu - tunaambiwa tabasam au kucheka kwenye uso wa ndugu yako muislam sadaqa😊 mimi kila siku nakutafuta mtandaoni Nipate kucheka umetufundisha Mahamri 😅namengi Jazashi'Allah kil'kher 🤲 Tuseme Alhamdulilah rabil'alamin kwa kila hali. Go ahead dear Allah karim - big hug with Love ❤️🌹
Shukran Jamila... alhamdulillah MEM ametufundisha dini, Imani kwa hivyo we try our best but as a physician you can't help but feel sorry for elderly patients who just want somebody to talk to or have been abandoned by their families or countless people with depression and suicidal idealities..the basis is all loneliness. Thank you for bringing awareness to this topic. We love your videos. Mandaazi is not the same as mahambri. Regards from Virginia. Watu huku udegene utetene..love from Lamu
Kweli maneno yako habibty... I can clearly relate to what you are saying sister.. It's not easy but that is life alhamdulillah na kila kitu ni makatib... Waarabu wasema "al ghurba saa'ba'" ugenini ni ngumu si rahisi... Mimi huondowa upweke hasusan nikiwa peke yangu nyumbani kwa kuskiza utube darsas za different shuyukh one of them ni sheikh Izzudin na jokes zake at times😅 huwa najskia niko home away from home😂 na naskiza kwa sauti ya juu kama vile radio.. so huku nafanya my house chores na huku naskiza durus nafaidika at the same time alhamdulillah... this is how I find relief and content in my heart😊 Be strong habibty and remember you are not alone Allah is with us all😊 Sending dua'a and hugs your way❤
Kwanza nakupa pole kwa maisha ya ugenini.Insha Allah Mola akujalieni kipato hicho mlokiendea.mkifanikiwa basi rudini kwenu.mtu kwao.hayo si maisha 😮. hususan kwa watoto.Subhana Allah .fikirieni kuna kesho mtaulizwa wachungaji.nini ulichokichunga.dada angu jiandae.
Naam Kabisa na siye wengine tuko km miji ya huko kuwa na Allah Subhaana ❤ Kila wakati dini imekupangiya mpangiliwo wote WA siku nzima unatakiwa Nini ufanye Ili ufarijike ukitaka mzungumzaji kuraani inakutosha Alhamdulillah una Mume watoto dini liislaamu ❤ ni neema kubwa tuliya jipumzishe neema kubwa halikufiki jambo ila limekadiriwa maisha ni mpangiliwo upumzishe Moyo upumzike una sehemu yake ridhika na ushukuri mengine ni makubwa zaidi yetu siye tuseme Alhamdulillah tumuachiye Allah Subhaana vna viumbe wake In Shaa Allah
Maa shaa Allah angalau nimekutana na msg ya maoni yangu. Ttzo wengi wao hua si wenye kujishughulisha na dini na hata uchaguzi wa marafiki. Nchi hii ukiikosea mtihani!!!
Ninkweli unayosema watu wetu wakisikia fulan yupo amerika wao waona yupo jannat firdous hawajui maisha ya huko yalivyo Allah atawastir daima dini na ibada ndio silah ya muislam quraan itawakinga na kila shari Allahuma Amin
Ni kweli kabisa upweke na faragha ni kitu kibaya Sana.. Mimi mke wangu kasafiri miezi minne tu basi unaona upweke Sana Ile siku yake ya kurudi unaiona mbali ni kwa sababu nchi za nje hizi upweke unakuwa mkubwa Sana.. Labda upate mambo ya kujibabaisha labda mazoezi kwenda mpirani.. Allah atupe nguvu na subra
Na nyie mnaojitia hamna haraka ndio number moja kwa kuvuruga akili za jamaa zenu. Mana wengi wenu mmekaa huko mara niletee I phone 14 pro max wkt mwenzio hata kuijua haijua, Mara mnadai viwango vikubwa vya pesa na kusingizia majanga Mara umeezukiwa na bati Mara unauguliwa, Mara hli Mara lile, Mara mnawadanganya kufanya biashara mnawadhulumu Mara wanakuaminini muwajengee mnawadhulumu na kuwajengea vibanda mitaa ya ng’ambu na kuwatumia picha za nyumba za mitaa ya ghali au mnazila kabisa pesa zote hakuna hata kibanda mnaongezea wake au mnalia samaki wanene.
Nchi hzi upweke upo lkn ukiutaka kwa sbbu mambo yapo mengi yakufanya. Misikitini darsa za kusoma/kujifunza Qur-an na pirika tofauti zpo, kazi za ndani ya nyumba zinakutosha pia si kidogo na hatuna wafanyakazi, km waisilam pia kujitahid kusoma Qur-an na kuhifadhi japo sura ndogo ndogo, kazi za kuajiriwa zimejaa za kufanya ujipatie pesa nk, sehemu za kutembea na wtto au km hamna pia zimejaa! Upweke unatoka wapi????? Mm nahisi inategemea na maisha uliotokea Afrika, ikiwa ulikua mtu wa vibaraza, umbea utaona upweke lkn km ulikua mtu wa pirika zako mwenyewe hujisikii upweke.
Pole sana na Hongera Kwa kuwajuza wale wote wenye Tamaa ya kufika huko! Kwa uelewa wangu kila kitu kina Hasi na Chanya, huko pia kuna Hasi na Chanya, na huku kwetu kuna Hasi na Chanya, kama kuna changamoto hiyo huko basi chukua yaliyo Chanya ya huko na uyaache yaliyo Hasi na ikiwezekana kuchukua yaliyo Chanya , baadae pima mwenyewe Hasi na Chanya za nyumbani Afrika na za huko Bora wapi, halafu chukua hatua! Kumbuka Tu waswahili wanausemi wao kuwa " mwenda kwao si mtumwa ", na wazungu pia Wana usemi wao "Go East, West, South, North , but home is the best"
ASALAM POLENI SAANA NDUGU ZETU MLIOKUWA NJE KUMBE MNACHANGAMOTO SAANA ALLWAA ATAWANUSURUU . CHA ZIADA SWALA NA DUA . MAISHA NDIO YANAYOTUHANGAISHAA ALLWAA KARIM
Hakuna mahali nimetaja maneno uliyoyasema wewe, SoubhanaAllah kumshutumu mtu ni vibaya au kuchanganya waliokuwemo na wasiokuwemo pia sio Sawa. Allah atusameh in Shaa Allah Ameen
@@jkizondoswahilibites434.Kasema wengi lkn sio wote. Na hlo alilolisema lipo. Tuishini kiisilam na tutafute marafiki wa kiisilam wenye tabia nzuri akili zetu ziondokane na kutawaliwa na shaitwani. Mm nashauri sana hayo pamoja na kutafuta marafiki wa mataifa mengine ambao wanadini, imani na upendo wa kweli. W’ke wa nyumbani wengi wao akili zetawaliwa na hasad na ushaitwani. Hata ushauri hawana mana km huku Ulaya unakuta w’ke wa nyumbani wengi wao wanavuta waume zao huwafundisha waseme hawana waume au wenyewe wanapenda kufanya hayo huwaambia waume zao. Ssa ikiwa m’ke anaakili hzo za kuvuta unategemea atakushauri nn??? Ikiwa hata mwenyewe haki zake za kujuilikanq ndani ya nch kua anamume hazitaki.
Watu wengi sana wanawekeza lkn mnawadhulumu, na wengine mnawapa mizigo mingi sana kwa kuwakusanyia mttzo ya uwongo mara Leo bati limeizuka nitumie pesa Mara mtto anaumwa, Mara hli Mara lile ilimradi wengi wao unakuta pesa kuieka si rahisi km mmemfunganishia chuma ulete/mana akipata mnajua mnaziagiza kwa kujipachika majanga au kumlaghai kibiashara. Unakuta mtu awe na akili sana nchi hzi ndio aweze kueka pesa mpaka akiamua kurudi afanye mwenyewe la maana. Mana hata mkitumiwa na mwenyewe yupo huku mnakula na kufanyia yenu.
Unakuta mtu anakupangia mipango ya kupata millions lkn ukimpelekea pesa anakwambia biashara imeharibika hii hasara tupu wkt pesa ushamkabidhi na ashazivuruga au kishafanyia yake. Hata ukimpa mtu mtaji atafute daladala ili ajiweze basi pesa ya kupelekea garage ikiharibika atataka itoke kwako. Acha watu wazeeke alipowapangia Allah usiwape stress! Huezi kujua ya mbele yako naww unaeza kujq kizee huku! kuja kizee huku km Mungu kakupangia. Muombe Allah kile unachokipenda na hakuna ufundi wala ujuaji, maisha yetu yapo mikononi mwa Allah! Anapopataka yy ndio utapopaishi na asipopataka huishi!!!! Usistress watu na wala usiruhusu mtu kukustress kwenye jambo ambalo lipo nje ya uwezo wako! Muamini Allah na muombe Allah na muachie yy Allah!