Naibu Waziri wa Katiba na Sheria) leo tarehe 5 Julai, 2024, ametembelea banda la Wizara hiyo na kujionea utoaji wa huduma za Msaada wa Kisheria zinatolewa kupitia Kampeni ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign).
Akiwa katika banda hilo lililopo katika viwanja vya maonesho vya sababa Wilayani Temeke Jijini Dar es salaam, Naibu Waziri Sagini amezungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma hiyo, kusikiliza na kutoa msaada wa utatuzi wa changamoto zao.
Ametoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya sabasaba kwenye banda hilo kwakuwa kampeni hiyo pia imekuwa ikitoa ushauri katika changamoto mbalimbali za masuala ya kisheria ikiwa ni pamoja na kuyamaliza kabisa.
Amesema mpango wa Wizara ni kuhakikisha ndani ya mwaka mmoja na nusu Mikoa yote inafikiwa na hudumu ya hiyo.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa kitengo cha huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi Ester Msambazi amesema mpaka sasa Kampeni hiyo imeshafika katika Mikoa 7 na kufikia zaidi ya Wananchi 495,000 ikijumuisha Wanawake, Wanaume, Watoto na makundi mengine mbalimbali ambao wamenufaika kwa kupata Elimu, ushauri na wengine wamesaidiwa kwenye utatuzi wa migogoro mbalimbali
4 июл 2024