Shangwe limeibuka Bungeni mara baada ya Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson kuwatambulisha Bondia Selemani Kidunda aliyeingia Bungeni na mkanda wa ngumi, Mwanariadha Alphonce Simbu pamoja na Mabondia wawili wa Tanzania Yusuf Changarawe na Kassim Mbundwike walioshinda Medali kwenye mashindano ya ndondi ya Jumuiya ya Madola.
Wanamichezo hao waliotambulishwa Bungeni leo Jumatano, Mei 24, 2023 pia ni maafisa wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
3 окт 2024