Hakika Prof. Mtembei Hakika tumeendelea kujikolonisha katika nyanja nyingi ingawa lugha hubeba utajiri wote wa jamii. Nimekuwa nikitafakari juu ya ukoloni hata katika kutatua changamoto za Kiafrika kwa kuamini kuwa mataifa ya Kimagharibi yatatusaidia. Jambo ambalo si sahihi kwa mtazamo wangu. Hakika mawazo haya yakibebwa na Nadharia ya Uzuu yanajadiliwa kwa ufasaha kabisa. Afrika tuamke na kuanza kutumia lugha zetu kuwasilisha maarifa mbalimbali hasa lugha yetu tamu nanpendwa ya Kiswahili❤❤❤
Kujikolonisha kwingine ni hiki kinachoitwa scholarship ambazo kwa mtazamo wangu zinalenga kuwachukuwa vijana wetu wenye uwezo mkubwa ambao wanatarajiwa kuwa ndio wasimamizi wa mambo yetu baadae wanachukuliwa vijana hao kwenda kulishwa na kuaminishwa ya huko wanakoenda kiufupi ni wanaenda kutengenezwa kwa mujibu wa mahitaji ya mtengenezaji