Wazanzibari ni Watu Mwenyezi Mungu amewapa Subra kubwa sana. Baada ya Dhulma zote walizofanyiwa na kuendelea kufanyiwa hiyo siku ya kuuliwa Watu na miaka yake ya Sabini kwa vifo na mateso ambavyo hata Firauni hakufanya na hiyo Miaka ya Dhulma ndio imekuwa ndio maadhimisho na Furaha na Vifijo ya kitaifa. Zanzibar ndio Nchi peke yake inayoadhimisha kwa furaha na maadhimisho ya Mauwaji ya Raiya wasiokuwa na hatia kwa kisingizio cha kuwazulia uongo wa Ukabila na Rangi na ati Ukoloni watubwasiokuwa na hatia. Hayo yaliyoandikwa kwenye vitabu vilivyoandikwa ni kidogo na madogo na ndio angalau yanaweza kuandikika lakini yapo mengi na makubwa sana ambayo watu wameyaficha ambayo hayawezi kuhadithiwa kwa jinsi yalivyokuwa Makubwa ambayo imma watu wameona wayanyamazie au hayawezi kuhadithiwa au yaliyowafika tayari wapo mbele ya haki Watu hujuta kwa maovu waliyofanya Wazee wao lakini Madhalimu hutumia Dhulma kuwa ndio silaha ya kuendelea kuwadhulumu watu na siyo kuwa kila mwaka siku ya Dhulma na matendo yake na tija zake ikawa ndio siku ya kuadhimisha na kutonesha watu Vidonda. Naona sitoweza kumaliza kuandika , bora niishie hapa. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hicho kidogo ambacho wametokea Wazee wetu kukiandika ambacho zamani ilikuwa siyo rakhisi na sasa wengi wao hawapo tena Duniani. Zamani wacha kuandika, Mtu kuzungumza tu dhiddi ya Serikali au Dhulma basi chembelecho wenyewe wana wa Mapinduzi Utaku.... Ndooni Haki na Ukweli utafichwa lakini daima unakuwa upo na ipo siku lazima utajulikana Ahsanteni
Ndio maana Zanzibar (Unguja na Pemba) haikai sawa wala haina barka kwa dhulma na mabaya walofanyiwa. NCHI imejaa watu lakini hawaijuwi nini Zanzibar na wangeijuwa kweli Zanzibar basi wote wangekimbia.
Kama pataandikwa mwisho wa watesaji kina Mandera itakuwa ni somo tosha . Nakubaliana na wazo la muandishi alomuandikia sh. Mohammed said. Na wewe kaka Mohammed Ghasan ulisimamie hilo.
Inauma na inasikitisha mnoooo la kushangaza mpka leo yanaendelezwa licha ya watu kushinda kwenye vibla vya misikiti kila ijumaa lkn wanaendeleza mauaji mabakaji na ulawiti kila siku za uchaguzi zanzibar na wakubwa hawasomi
ukweli huyu msomaji wa qaswida hii ndio aliumia zaidi na nimefanya uchunguzi anakasida nyingi na nzuri na hana makuu lakini jamii haioni hizi kazi zake kwa jina anaitwa Sheikh Issa Qaswida nimepekua youtobe yake huyu kija sio wakawaida
Sultan Said Khalifa aliifnyia makubwa Zanzibar japo kuna watu fulani wanadai alikua Kibaraka, Jee hawa viongozi walioko leo ambao 'sio vibaraka' wamewafanyia yepi waZanzibari ???????????
Kitu kinachonikwaza na kuniuma hadi waleo ni kwanini Sultan Jamshid Al Busaidi na Mohd Shamte waliuza mwambao kwa nchi ya Kenya bila kuhusisha watu wa mwambao (Mombasa) wenyewe na kutuletea madhila makubwa kwa kupoteza ardhi zetu, biashara, tamaduni, na kadhalika hadi leo hii 😢😢😢😢
labta haijulikani llipo, wanahistoa wote afrika mashariki ,hamjagika kilwa , itakua maajabu ,ya wanahistorua wa ajabu ulimwengu , ngombe kilwa inatarehe mlangoni mpaka Leo, 1123,hijiria