Uwamuzi wa ovyo sana... Ni ujinga Sanaa.. Tulishasema mnapojenga BRT ongezeni lane za barabara ya kawaida ziwe tatu Kila upande... Hakutakuwa na aja ya BRT sasa... Bora kupanda daladala sasa... Mnaenda kusababisha foleni kwenye BRT... Akili ya ovyo..
Tuweke nguvu kutengeneza barabara mh waziri ukiruhisu mwendo Kasi itumike ndivyo sivyo baada ya wew kuondoka atakayechukua kijiti yeye ataleta bajeti ya kuanzia kurepair izo barabara tutaendelea kurudi nyuma Ukweli foleni inaudhi na kipindi Cha mvua na joto ndo balaaa ila muiche iyo barabara mtanue na kuweka ringroad ili na mji uwe msafi
Ajari zitakuwa nyingi sna weee mwendo kasi hakuna hata bamsi yaaan watakuwa wanagongana kila cku waache hivyo hivyo tu mwendo kasi ipite mwendokas yenyewe
Wanazingua sana, wanavyojenga mwendo kasi tulitakiwa tuwe na njia nne au nane kila upande sababu ili jiji linakuwa sana huwezi weka njia mbili kwa watumiaji wa kawaida lazima zitazidiwa tu, ili jiji barabara zinatakiwa zipanuliwe ziwe pana, lakin serikal hawafikilii miaka 10 mbele itakuaje! Wazo la waziri ni bovu na wakiruhusu hizo gar hawataweza kizicontrol kati ya mwendo kasi na zakawaida hata siku Moja, itakuwa ni mwendo wa vurugu, yaan tutaonekana ni wajinga sana
Ili kutibu tatizo la foleni na msongamano linalozidi kukuwa Dar es Salaam, Ni muhimu Serikali ikaifungua ile miji mikubwa mingine kwa kuweka huko Vivutio Vikuu kama vya Dar au hata zaidi. Ikazitanue barabara za miji mingine na kuanzisha barabara za ndani nyingine mpya, na hasa hasa ile miji mikubwa a.k.a Majiji. Ikajenge huko katika hayo majiji madaraja, barabara za interchanges, flyovers na njia za ma-bus ya BRT. Bila kusahau kuweka vivutio mbali mbali kwa kuhamasisha uwekezaji kutoka ndani na nje wa Viwanda na biashara, Sanaa na Michezo n.k. katika miji hiyo pia.
NI WAZO ZURI SEMA MAANA YA MWendo kasi itaondoka kwa sababu hata malori yatatumia barabara hiyo mwishowe unakuta gari limezimika na kuziba mwendokasi na kuzidi ongeza changamoto, ni bora mruhusu dala dala tu ndiyo zitumie hiyo barabara kama test hapo tutaweza punguza pollution na foleni mjini.
Hapo ndipo huwa tunafeli Tanzania. Sasa hii maana yake nini? Badala ya kuongeza mabasi ili huduma ziwe nzuri na watu waache magari nje ya mji..wewe unahamasisha waanze kutumia hii barabara?
Huo ni upuuzi, kila siku watu wanasema barabara za pembeni wekeni njia tatu au nne kila upande, lakin nyiny bado mnaweka njia mbili kwenye Jiji ambalo linakua kwa kasi, kila kukicha watu wananunua magari, sijui viongozi wa juu wanafikirikia nin? Barabara ya kutoka airport kuja posta ni pana sana mngeweza kuweka hata njia nane, yaan nne kwenda nne kurudi kwa watumiaji wa kawaida, yaan mnachokifanya nyiny ni mnajenga vile vile kama zaman isipokiwa ni mnaongeza tu mwendo kasi kati, lakin hiz barabara hazitoboi hata miaka 5, zitazidiwa tu, mwisho wa siku itakuwa tunapanua barabara kila siku ujenzi auishi.