Miaka minne tangu kutokea kwa shambulizi la kigaidi katika eneo la Dusit D2, Riverside Nairobi lililosababisha vifo vya watu 22, makovu ya waathiriwa yameendelea kama tukio la hapo jana. Hata hivyo, kwa mama Sakina Mariam, makovu yake sio la kawaida kwani mwanawe wa kiume Ali Gichunge alikuwa mmoja wa magaidi waliotekeleza shambulizi hilo. Kwa mama huyu maisha yake yamebadilika na uchungu alio nao ni kuwa siku moja atapata fursa ya kuwaomba radhi waathiriwa kwa ukatili wa mwanawe. Gatete Njoroge alikuwa Isiolo na kutuandalia taarifa hii maalum
14 янв 2023