Ajiuzulu hata Ubunge, apishe siasa zetu anazichafua! Hafai hata kuwa balozi wa mtaa,hawezi kutufikisha mbali huyu kijana. Awali nilisema ni namna alivyozaliwa na kukulia!
Alichokisema Nape ni uhalisia wa kinachofanyika, ila tatizo ni kusema hadharani. Unapokula na kipofu usiseme unavyomdhurumu yaani usimshike mkono, bali endelea tu kumdhurumu kimya kimya. Kumwondoa ni kuweka kizibo kwenye chupa iliyo na uchafu ndani ili kuondoa harufu iliyojitokeza nje. Bora uchafu ubakie tu ndani ya chupa. Wapiga kura wanatumika kama maigizo tu, lakini uchaguzi ulishaamriwa nje ya kura. Sasa anaeyasema yaliyojificha lazima aondolewe ili kipofu azidi kudhurumiwa kwenye chakula cha uchaguzi kwa amani bila kuguswa mkono. Lakini labda pengine Mama hana siasa kama za watangulizi wake. Hebu tusubiri.
Huwezi kuamini ktk 4R na falsafa ya goli la mkono pamoja. Falsafa za lazima tushinde kwa kishindo hata kwa dhambi haziendani na falsafa ya 4R hata siku moja.
Rais wangu Samia, natofautiana sana na Peter Madeleka kwamba eti Rais hupendi goli la mkono yaani eti Rais unapenda haki, Rais ungekuwa hupendi goli la mkono(USHINDI HARAMU). INGEKUWA HIVYO BASI, TANGU ZAMANI UNGEKUWA UMEISHA TUPATIA KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI INGEKUWA NI KINYUME NA SASA!!! NDIVYO NINAVYO AMINI. NINACHO KIONA HAPA NI HASIRA YAKO KALI JUU YA NAPE NA KAULI YAKE KWA KUWAMBUA KWA TENDO HILI HARAMU LILILOPIGIWA KELELE SANA NA WAPENDA HAKI KWA MIAKA MINGI TANGU 1995!!! RAIS WANGU UNALIJUA HILO. BILA SHAKA YOYOTE NAAMINI KAULI YA NAPE IMESABABISHA HII TEUA TENGUA YAKO!!! MWISHO NAMWOMBA MUNGU AKUPE HEKIMA YAKE YA KUTAMBUA KUWA KAULI YA NAPE NI BOMU LA ATOMIC KUELEKEA CHAGUZI ZILIZO MBELE YETU, RAIS WANGU USIITEGEMEE KABISA KAULI YA MZEE MAKALA YA KUIKANUSHA KAULI YA NAPE KWAMBA IMEKUBALIKA, LA HASHA WAPENDA HAKI WAMEIAMINI KAULI YA NAPE SI YA KAULI YA MAKALA!!! MUNGU AKUONGOZE AKUPE HEKIMA UTAMBUE KUWA USALAMA WA NCHI HII UKO MIKONONI MWAKO KABISAA SI MWINGINE AWAYE YEYOTE KATI YETU SOTE ZAIDI YA MILIONI 60 KAMA HUKUWAHI KUONA NA KUFIKIRIA UMUHIMU WA KUTUPA KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI BASI FIKIRIA SASA KUTUPATIA KABLA YA CHAGUZI ZILIZO MBELE YETU, HASA NI KUTOKANA NA KAULI YA SASA YA NAPE TOFAUTI NA YA ZAMANI YA GOLI LA MKONO HAKUIDADAVUA YA SASA AMEIDADAVU NA WATU WENGI NDIVYO WANAVYO AMINI!!! USISAHAU KUWA KURA NI MALI HALALI KAMA MALI NYINGE YOYOTE ANAYOIMILIKI MTU KIHALALI!!! KWA MUJIBU WA MITANDAONI SAUTI ZIMEPAZWA ZIKITOA WITO KWA WAPENDA HAKI KUZILINDA KURA KWA HALINA MALI. RAIS WANGU SI KAULI ZA KUPUUZWA KIRAHISI RAHISI TU. NIKIWA MWANA NCHI WA KAWAIDA NIKO CHINI YA MIGUU YAKO NIKIWA NIMEJAA WASI WASI JUU YA MSTAKABALI WA AMANI YA NCHI YETU!!! MIMI NINA AMINI KUWA MLINZI WA AMANI NI HAKI BASI, WALA SI MTUTU WA BUNDUKI. NAKUOMBA KWA UNYENYEKEVU WAPE HAKI YAO WANANCHI WAKO NCHI IWE SALAMA. MUNGU IBARIKI TANZANIA YETU.