Mateso mengi ya familia unayopitia chanzo chake sio wewe,unachokutana nacho ni matokeo tu ya kile kilichosimamishwa kwenye misingi ya familia. Msingi uliowekwa ndio unatengeneza matokeo katika ulimwengu wa mwili.Na siku zote adui kabla hajakuvamia huchunguza kwanza msingi uliotokea maana ndio unaoweza kumpa backup ya shambulio lake.
Mfano: Kama kwenye msingi wa familia walisema kuwa watu wa nyumba hiyo hawatokuja kuingia kwenye ndoa,ukivamiwa na roho ya jini mahaba ni rahisi sana yenyewe kukutesa kwa sababu msingi wa familia uliyotoka unampa backup ya kutekeleza azma yake.
Ndio maana kwenda kwa Mungu na kumuomba akuvushe eneo fulani bila kujua chanzo cha hiyo changamoto ni nini ni ngumu sana kuona majibu.
Daudi alisema, Misingi ikiharibika mwenye haki atafanya nini?
Hata kama unaishi kwa haki lakini kama hujarejea kwa Mungu kwa rehema ili ahusike na hiyo misingi ni rahisi sana ukazidi kuingia kwenye changamoto kila siku.
Ni muhimu sana kutengeneza na Mungu ili nafasi Yake kwenye familia uliyotoka iweze kurudi.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our RU-vid: www.youtube.co....
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz
and Subscribe Pastor Sunbella Kyando RU-vid
/ @pastorsunbellakyando
6 окт 2024