Mzungu mmoja wa Marekani amewashangaza wengi katika kaunti ya Siaya kwani yeye ni mchuuzi wa keki anazozipika mwenyewe katika mtaa wa Siaya. Mwanaume huyu ambaye ana umri wa miaka 48 amewaacha wengi vinywa wazi haswa kwa kuwa biashara ya uchuuzi inanasibishwa na watu wenye mapato ya chini. Hata hivyo kama tulivyogundua ni kwamba mwanamume huyo aliingia bishara hiyo ili kuwanaifaisha wengine.
5 авг 2014