Ninapenda kuwashauri watanzania wenzangu tusiwe sana tunamapenzi ya hovyo kumpenda mtu bila kuona athari na faida zake ,ni kweli watanzania tumechoka na tunahitaji mabadiliko, lakini swali ni nani kwa dhati na matendo yake yanaonyesha kutujali sisi watanzania tofauti na kujijali yeye na wenzake wachache?, hivi kweli unaweza kumpa nchi Mbowe ? Au Tundu Lisu ? au Zito?nani hasa atakuwa afadhali ya huyu kuliko tulie nane kwa sasa? Hakuna kabisa ni kwamba tukifanya mabadiliko kwa lazima tu kwamba hawa wametuchosha tumpe yeyote litakalo kiwa na liwe ? Watanzania tukumbuke maneno ya mwalimu Nyerere nchi sio ya kufanyiwa majaribio ni hatari tumeshawaona hawa tumewapima kwa ubunge wamefanya nini kweli hayo waliyokuwa waliyafanya yalikuwa na usalama kwetu? Zaidi ya kuhubiri nchi isitawalike maandamano fujo hayo ndio tunataka? Ni bora tuendelee kuwarekebisha hawa iko siku tu atatokea mmoja wa kutetea na kulinda masilahi yetu ,au kitatokea chama chenye misingi mizuri ambayo tutaziona na tutawapa nchi ,HATA FIRAUNI MUDA WAKE ULIISHA AKAJA MUSA NA KUMLEA YEYE MWENYEWE AKAWA MKOMBOZI , TUWE NA SUBRA tuachane na hawa wahuni mamluki wasaliti hawafai hata bure
Iv kwel wew unajua kuchambua kitu kwel na kama hawa watu uliowataja unaweza kutueleza makosa yao ili na sis utufumbue macho au na wew unaandika andiko la uchawa tu hakuna lolote
Chadema wamejitahidi sana Watanzania ndo hawaelewi. Huu c wakati wa kuwalaumu wamebeba maumivu mengi sana. Wananchi nao wabebe jukumu la kuitetea nchi yao ndo maana wanarudi kwa wenye nchi.
Huyu jamaa ni mjinga kweli😂. Hivi wangapi walihama CHADEMA? Akina Kitila na wengine wengi tu. Kisha unasema hakuna aliyetoka CHADEMA? Guys ninyi ni waandishi wa aina gani?
Unapokuwa kiongozi unapoteza sifa ya kulalamika... unatakiwa kutenda katika hoja iliyopo... Vyama kila siku vinalalamika tuu....vinalia lia tuuu..... Tutatatuaje matatizo ya kijamii kwa kulalamika tuu
Wapendwa njaa mbaya maana inaweza kukufanya mtu mzima ikaonekana debe tupu. CDM muendelee na utaratibu ns mipango yenu wananchi wako nyuma yenu. Tuna mashaka katumwa mtu kuokoa jahazi wakati huu wa uchaguzi ili kupunguza nguvu za CDM. CDM kaeni macho na hekima
Mmemwambia ukweli sabab kuna wakati anaguswa na wananch ila na Kuna wakati aguswi akiwa ktk nafasi fulan pia maneno yake yanabadilika kutokana na Hali ya upepo
Mimi nadhani tujikite kujibu hoja za Dk. Slaa. Wengi mliopo hapo sina hakika kama mmejibu hoja za Dk. Slaa, wengi mnasema tu kuwa eti kwa nini hakusema alipokuwa huko CHADEMA?
Watanzania wenzangu! dr slaa hizo ndiyo njia zake za kujaza tumbo lake! kila uchaguzi mkuu unapo karibia huwa anabadilika na kuwa kinyonga kwa kuwabagaza wapinzania wa vyama vya siasa ktk nchi hii hasa chadema! anafanya hivyo kwa maslahi yake binafs! uchaguz ukisha kwisha unabadilika tena na kujifanya mpinzani! huyo ndiyo Dr slaa halisi.
Muwe mnatumia akili kidogo...Nyinyi hapo mnaongea kama wakina nani...ndivyo hivyo hivyo Dr Slaa nae anaongea. Chadema ili iimalike lazima iambiwe ukweli ...Dr Slaa ameongea ukweli achaneni na habari za nyuma mbona hata wakina Wasira walikuwa upinzani...kuweni na akili kidogo...Alafu hakuna uchaguzi Tz ulishawai kukubaliwa na wapinzani kuwa umekuwa uhuru na haki na hautokuja kutokea eleweni ili.