#jumajux #carenbujulu Unaipenda kazi yetu na ungependa kutuunga mkono? Sasa unaweza kutuchangia kiasi chochote kuanzia shilingi 500. Fuata link hii hiveticket.web... Tunashukuru kwa kuwa Mwana SnS unayejali
Pia maneno Waga❌ au huwaga❌, si Kiswahili sanifu. Tumia neno HUWA☑ kwenye sentensi zako, na wote wanaotumia hayo maneno ya awali. Aidha msiongeze "ga"❌ mwisho wa maneno yaliyokamilika. Mfano Nakupenda ☑ sio nakupendaga❌. anakujaga❌ wakati inatakiwa kusema huwa anakuja☑, kama hilo neno nasemaga❌, usahihi wake "huwa nasema" ama "mara nyingi nasema au mara kwa mara nasema ☑n.k
Wasanii mnatakiwa kuongea lugha sanifu, hasa kwa hilo jina lenu la kioo cha jamii, Nakusahihisha "si nyimbo inafanya vizuri" ulitakiwa kusema "wimbo unafanya vizuri". Nyimbo (nyingi) ni wingi wa neno Wimbo (mmoja) Hapo dakika ya 2:11 nakusikia umechanganya maneno yote mawili kwa maana moja. Yani hujafahamu tofauti ya hayo maneno. Hebu jamani tujitahidi kunyoosha kiswahili chetu, sisi Watanzania ndio wenyewe linapokuja suala la lugha hii adhimu, watu wa nchi jirani na duniani wanajifunza kutoka kwetu.