Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati, Dkt. Doto Biteko amesema mtambo namba saba ambao ulikuwa katika majaribio sasa umeingizwa katika Gridi ya Taifa na kufanya idadi ya mitambo inayozalisha umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere kufikia mitatu ambapo kila mmoja unazalisha megawati 235.
Ameyasema hayo alipotembelea mradi huo ambapo amesema mtambo namba sita nao upo katika majaribio ambapo jitihada hizo zinafanywa ili kuhakikisha nchi ina upatikanaji wa uhakika wa umeme.
✍@official_jennifersumi
#azamnewsupdates
29 авг 2024