Mtangazaji wa kipindi cha Mshikemshike Viwanjani, Hasheem Ibwe usiku wa kuamkia leo amefunga ndoa na Nasra Ally Salim katika msikiti wa Shekhat Hisa uliopo Magomeni jijini Dar es Salaam.
Ndoa hiyo ilifuatiwa na sherehe ya ndoa iliyofanyika usiku huo ikijumuhisha ndugu wa pande zote mbili za bwana na bi harusi na baadhi ya wafanyakazi wa Azam Media ambako anafanyia kazi bwana harusi.
15 окт 2024