Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika ametoa raia kwa Watanzania kujitokeza kujiandikisha na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajia kufanyika Novemba 27, 2024.
Mnyika ametoa raia pia kwa mamlaka zinazosimamia uchaguzi huo na chama tawala kujiepusha na michezo michafu itakayopelekea kuharibu uchaguzi. Sambamba na hilo amewataka wanachama wa CHADEMA kujitokeza sasa rasmi na kutangaza kutia nia katika zoezi hilo.
11 окт 2024