Nikiwa miongoni mwa washiriki wa Uimbaji huu dayosis mwaka jana nikiwa na kwaya yangu ya asili ya kimasai (.....) Tulikuwa wa 3 kuingia jukwaani . Pia mimi ni mwimbaji wa Noten na (mkaguzi wa sauti pia) hii kwaya ilistahili no 1 kwa sababu mbili za muhimu, 1. Kwanza Wanaimba kulingana na muda (karne) wabunifu mno na wameimba asili kisasa zaidi mtu yeyote hata asiye masai anaweza iskia na asiwe na maswali kichwani. 2. Mwalimu wao anajua na walikuwa wakamilifu katika uimbaji wao yaani kwanzia vitendo hadi matumizi ya sauti🔥🔥🎤