Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli leo tarehe 21 Julai 2018 akiongozana na mkewe Mama Janeth Magufuli, amefika Msasani jijini Dar es salaam nyumbani kwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete kutoa pole kufuatia kifo cha Mkwewe Mzee Rashid Mkwachu.
Marehemu Mzee Mkwachu ambaye ni baba mzazi wa mke. wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, alifariki dunia tarehe 19 Julai 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam
12 сен 2024