Roho ya umaskini haikuzuii KUNENA kwa lugha, lakini itahakikisha kwenye eneo la fedha hausogei.
Kilichomfanya huyu mtu atoke kwenye makaburi ni kwa sababu ya uwepo wa Yesu, Ulimuhamisha kutoka sehemu ya mauti aliyokaa muda mrefu.
Kuna watu kwenye ulimwengu wa roho wamehamishwa na kuwekwa kwenye location(maeneo) ambapo wakiwa kwenye hayo maeneo chochote wanachokifanya KINAKUFA.
Shetani ili afanye uharibifu kwako huhakikisha kwanza amekuweka kwenye eneo ambalo anapata access na wewe wakati wowote akihitaji, vilevile huhakikisha wale ambao ni msaada kwako anakutenga nao.Ndio maana kuna aina fulani ya watu kila wakija karibu na wewe ndani yako kunainuka tabia ambazo hata hujui zimetoka wapi..kiburi, hasira iliyopitiliza,majivuno n.k na kipindi watu hawa wakiondoka unarudi katika hali yako ya kawaida.Na watu wengi jambo hili limewatesa sana kwa sababu hawajui chanzo ni nini.
Ukiwa kwenye eneo la namna hiyo kila atakaye kuja kwenye maisha yako ana tatizo kama lako,na ndio maana wewe na rafiki yako wote mnapitia changamoto zinazofanana.
#PastorSunbella#RohoYa#Umasikini
2 фев 2022