Тёмный

Salama Na ZAHIR ZORRO SE6 EP52 | KIMULIMULI PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460 

YahStoneTown
Подписаться 395 тыс.
Просмотров 19 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Zahir Ally Zorro ni mkongwe wa muziki wa dansi na kwa habari ambazo nimepata ni kwamba enzi zake alikua wa moooto sana tena kwenye kila nyanja, kuimba, kuandika, kupiga gitaa na mpaka uvaaji, alikua handsome boy sana na ulimbo kwa kina Dada enzi hizo. Utashi na ucheshi na u sharp wake ndo ambao ulikua unamfanya asimame PEKEE kwenye kadamnasi ya wanamuziki wengi wa kipindi hiko. Naomba nikukumbushe pia kwamba enzi hizo zilikua pia si za kuzichukulia poa kabisa, maana ushindani wa bendi na vipaji binafsi ulikua wa hali ya juu sana, na yeye kama yeye alikua moja ya wale WAKALI wa kipindi hiko. Kama muajiriwa wa Jeshi Mzee Zahir alikua shujaa wa aina yake enzi hizo za ujana wake, kama askari alikua akijituma na ndo maana hakua na cheo cha kinyonge, na kama muandishi na muimbaji na mpiga gitaa pia alikua na nafasi yake ya kipekee. Ukimuangalia hata rangi yake imekaa ki chotara na kwenye mazungumzo haya ana nikumbushia jinsi ambavyo Baba na Mama yake walikutana na ambavyo yeye alizaliwa. Interest yangu zaidi ilikua jinsi ambavyo yeye kama Baba ameweza kuwakuza watoto wake wawili ambao nao wamekuja kuwa wanamuziki wazuri tu tena, Marehemu Maunda Zorro ambaye alifariki mapema mwaka huu (Mwenyezi Mungu amsamehe makosa yake na Amrehemu) na Kaka yake Banana Zorro. Wakati wa kuanza Banana ndo alionekana kuwa angekua super star zaidi ila Maunda nae alipoikamata reli yake kila mtu alimfahamu vizuri. Malezi yao baada ya Marehemu Mama yao nae kutangulia mbele ya haki wakiwa bado wadogo naamini ilikua mtihani mkubwa kwa Mzee Zorro. Ila kwa Rehema za Mwenyezi Mungu Mzee huyo aliweza na ameweza kuhakikisha watoto wake wanakaa kwenye mstari ulio nyooka na kufanya mziki mzuri na kwa heshima na taadhima. Kwenye maisha yangu ya kazi hii nimeshawahi kukutana na Mzee Zorro ila hatukuwahi kufanya maongezi kama haya ingawa nyuma ya ubongo wangu siku zote nilikua nataka kufanya hivyo, na wakati mwengine nilikua nawaza hata ingekua viti VITATU upande ule yaani Baba na watoto wake wawili, kisha nikaona tutakosa kinaga ubaga nyingi, yaani hatutawafaidi sana kama tukiamua kufanya hivyo maana kati ya watatu hao kila mmoja ana story zake ambazo anafaa kupatiwa wasaa wake. Kwa bahati mbaya Maunda alitangulia mbele ya haki na wakati kwa upande wetu ulifika kwa sisi kutaka kukaa chini na Mzee Zorro ili tuyajue yake na kutaka kujifunza kutoka kwake. Mimi na Director wangu wa episode hii tulikua na wakati mgumu kiasi maana pengine tulitaka zaidi ya ambacho tuliweza kupata na hilo Mimi na Alex (Director wangu) tumekubaliana kwamba imetokana na kuondoka kwa Maunda, tunaamini toka Maunda amefariki Mzee Zorro hajarudi katika hali yake ya kawaida, na inaeleweka maana yule hakua tu Binti yake, alikua ni rafiki yake wa karibi saaaana pia. Mzee Zahir alikua analala na Maunda na Banana chumba kimoja mpaka siku chachu tu kabla ya Maunda kukua, na hiyo ilikuja baada ya Banana kumuambia Mzee wake kwamba pengine sasa umefika muda wa wao kulala tofauti. Ananiambia katika episode hii kwamba yeye waala hakua anaona tatizo lolote juu ya hilo maana wenyewe walikua wanaishi tu kwa upendo na maelewano ila baada sasa ya Banana kusema ndo hata yeye alipoona ni kweli muda wa kupeana faragha kwa kila mmoja kuwa na sehemu yake ulikua ushafika. Kwa mtu ambaye walikua wanaonana karibu kila siku na kuongea sana hata baada ya Maunda kuhamia kwa mtu wake ukaribu wao bado ulikua wa karibu sana. Mimi namuombea Mzee Zahir Ally Zorro wepesi katika kipindi hiki kigumu ambacho anapitia na In Shaa Allah arudi katika hali yake ya zamani ya ucheshi na bashasha tele na kwa hii ambayo tumeweza kufanya naye itakupa ufahamu wa kiasi wa legend huyu ambaye pia ni mjuzi wa mambo mengi ya historia na muziki wa jana na wa leo hapa ulimwenguni, ukitaka kuongea na Mzee Zorro hukusu culture ya Mexico, mabadiliko ya tabia nchi, timu ya Taifa ya Ufaransa, mapenzi ya Tabu Ley na Mbilia Bel yote atakua na la kukuambia. Special special human being. Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Развлечения

Опубликовано:

 

29 янв 2023

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 36   
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
67 years congratulations daddy 😘babu
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
Salama na Joel nanauka @joel nanauka 🙏😘
@ilhamsalum6815
@ilhamsalum6815 Год назад
Chana la ndizi limetulia dada hongera😍💞
@mohamededdi7527
@mohamededdi7527 Год назад
Whatching from Dublin Ireland. Salama tunakupenda.
@tikitakashow
@tikitakashow Год назад
quite inspiring Mzee Zoro is a legend @Salama Kindly bring Madebe Lidai enjoying from +254
@stevewanga957
@stevewanga957 Год назад
hii interview 2lingoja sana ..mkaipotezea ..thanks umeileta ...much love frm 🇶🇦🇶🇦
@YahStoneTown
@YahStoneTown Год назад
Karibu na endelea kuenjoy
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
Nampend sana baba maund zor baba banana zor
@rehemaothman2475
@rehemaothman2475 Год назад
Ma sha Allah mzee zahir
@fadhilihussein6580
@fadhilihussein6580 Год назад
Anajichanganya Mara singasinga mara mmanyema haeleweki jamaa
@allykabaang2309
@allykabaang2309 Год назад
Salama na Niki mbishi
@masturaabdul1007
@masturaabdul1007 Год назад
Tunamsubiri Juma lokole na wema sepetu.
@rehemaothman2475
@rehemaothman2475 Год назад
😅🤣🤣🤣Hapo kwa juma weeee na subiria
@musabichacha6541
@musabichacha6541 Год назад
salama eeeh tuleteeee masoud kipanya aiseeeee
@YahStoneTown
@YahStoneTown Год назад
Iko tayari, tutaiweka RU-vid hivi karibuni
@lowkeybongo
@lowkeybongo Год назад
Nikimaliza hapa naenda kuiangalia Nzela
@otienokhogallo6422
@otienokhogallo6422 Год назад
Salama na billnass bas
@YahStoneTown
@YahStoneTown Год назад
Stay Tuned. Tutaipandisha RU-vid hivi karibuni
@rashidrm5341
@rashidrm5341 Год назад
Salama naomba mlete shafiihdauda
@saumusalimuhassan2499
@saumusalimuhassan2499 Год назад
Ila Rafiki yangu umepungua, au ndio uzee.
@Chemba67
@Chemba67 Год назад
Dah Cassanova Masaki enzi hizo .......naitafuta safari ......wazungu walikua kibaO
@azizamohamed7692
@azizamohamed7692 Год назад
Nimewahi leo 😆😆
@mrfashion1687
@mrfashion1687 Год назад
Sasa nasubiri SALAMA NA MILLARD AYO, SALAMA NA MWIJAKU, SALAMA NA B12 .
@nellymatalanga5033
@nellymatalanga5033 Год назад
Millard na Sky Bundala
@nomamatata754
@nomamatata754 Год назад
Oooh for sure my nigga me too
@munampinda1888
@munampinda1888 Год назад
Wa pili leo wapi likes zangu
@hajiomary3766
@hajiomary3766 Год назад
Mm nasubir salama na mtiga abdallah🙏
@fatmaabdallah7709
@fatmaabdallah7709 Год назад
Hiyo miziki kwanini hamuzimi mnapomuhoji mtu?! Hamuoni inaharibu interview tunakuwa hatusikii vizuri
@frankfathertisa8907
@frankfathertisa8907 Год назад
Pls buy posds ambazo zina noise cancellation utanishur
@fatmaabdallah7709
@fatmaabdallah7709 Год назад
@@frankfathertisa8907 zinauzwa wapi kakangu?
@yahyahamad1802
@yahyahamad1802 Год назад
sasa nami nakushauri baba usivae hizo.cheni
@winnifridaashery4449
@winnifridaashery4449 Год назад
Zina nini angalia moyo wa mtu cyo mwonekano wa nje
@yahyahamad1802
@yahyahamad1802 Год назад
@@winnifridaashery4449 kwa Kua Anasema mwenyewe ni muislam sasa ni haramu mwanamme kuvaa mambo ya kike, na mwanamke kuvaa mambo ya wanaume
@abdulnaseermrisho4342
@abdulnaseermrisho4342 Год назад
@@winnifridaashery4449 hayo ya kuangalia moyo wa mtu na sio muonekano yapo huko kwenye ukristo wenu,waislam tunaangalia Muonekano na moyo wa mtu (Uislam ni unadhifu)
@issazalala4907
@issazalala4907 Год назад
Kwanza ongera kwakua kalibu na Mollah wako lakini ningependa kuona unaacha kuvaa hayo macheni nakama hauto jali achamziki utani samee kamanime kukwaza
Далее
شربت كل الماء؟ 🤣
00:31
Просмотров 14 млн
GABO ZIGAMBA AMEKUJA NA MOTO MWAKA HUU/ JIONEE
1:01
Просмотров 12 тыс.
Salama Na Madee Ep 18 | MPAKA MSHALE Part 1
40:33
Просмотров 67 тыс.
I meet Mr.Beast
0:15
Просмотров 10 млн
This or That 🛍️
0:52
Просмотров 6 млн