Habari Ashu K!! Nafahamu uchungu ulionao na majonzi yaliyopo moyoni mwako. Niliguswa sana na hali iliyotokea na nafahamu jitihada ulizokuwa ukizifanya katika kumuokoa Mzazi wetu lakini mapenzi yake mola yakatimia. MUNGU aendelee kukupa nguvu wewe, baba na familia kwa ujumla muda wote wa maisha yenu, MUNGU mwenye uweza ndie anaetoa faraja na matumaini hivyo MUNGU atawajaalia zaidi faraja. Tumuombee MAMA huko aliko MUNGU amrehemu. Nakosa maneno mazuri ya kukufariji, kila neno naona halifai, basi mola aendelee kuwajaza uvumilivu na amani. Asante. Albert Kapala (Mzee wa Kigamboni)