Muhimu ni kuwa na mtazamo chanya na utayari wa kuanza kidogo kidogo,nilichoelewa kuhusu nyasi lengo ni kuwa na kiwanda cha kuzalisha nyasi zilizofungwa vizuri na zinazoweza kuhifadhiwa kwa matumizi ya baadae. Hivyo mashine ya kukata nyasi ni sehemu tu ya mitambo/mashine katika kiwanda cha kuandaa malisho ya wanyama. Ukiwa na rasilimali majani na mashine za kuchakata majani (malisho ya wanyama) na kuyafunga, bila kujali sana kiwango cha teknolojia basi utaweza kuwa na kiwanda kitakachoweza kukusaidia kupata kipato kwa kuuza malisho ya wanyama kwa wakulima.